Wednesday 18 February 2015

Maandalizi Tigo Kili Nusu Marathoni 2015 yashika kasi





Mkurugenzi wa Michezo Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Leonard Thadeo akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa mbio hizo hivi karibuni, pembeni yake ni Meneja Chapa wa Kampuni ya Tigo ambao ni wadhamini wa mbio za kilometa 21 William Mpinga.
Na Mwandishi Wetu
 MBIO za 13 za Kilimanjaro Marathoni zinafanyika mjini Moshi Machi mosi mwaka huu na kutarajia kushirikisha wanariadha zaidi ya 800  kutoka nchi mbalimbali duniani.
Kila mwaka mbio hizo zimezidi kupata umaarufu mkubwa kwa washiriki, wadhamini na watazamaji kuzidi kujitokeza kwa wingi kila mwaka kutokana na umaarufu wa mbio hizo.
Mbali na mbio za kilometa 42, mbio za walemavu na zile za kilometa tano za kujifurahisha, pia ziko mbio maarufu za nusu marathoni, ambazo zinadhaminiwa na Kampuni ya Simu za mkononi ya Tigo.
Kwa mara ya kwanza mwaka huu Tigo watadhamini mbio hizo za nusu marathoni za Kilimanjaro na watatoa zaidi ya Sh. Milioni 80 kwa ajili ya shughuli mbalimbali zikiwemo zawadi kwa washindi.
Tigo kwa kushirikiana na makampuni mengine watadhamini mbio hizo za Kilimanjaro Marathoni, na fedha zitakazopatikana kutoka kwenye mashindano haya zitatumika kwa ajili ya kulinda mazingira yanayouzunguka Mlima Kilimanjaro.
Zawadi Kwa Washindi:
Tigo imetenga kiasi cha Sh. Milioni 10 kwa ajili ya washindi wa mbio za nusu marathoni. Washindi  wa kwanza upande wa wanawake na wanaume watazawadia Sh.Milioni 2 kwa kila mmoja, na tayari washiriki 5,000 wameshajiandikisha kwa ajili ya kushiriki mbio hizo za nusu marathoni.
 Pia kampuni hiyo itawadhamini wafanyakazi wake watano kwa ajili ya kushiriki mbio hizo za nusu marathoni.
MVUTO KWA WASHIRIKI:
Mbio za Kilimanjaro Marathoni zimeendelea kuwa kivutio kwa washiriki wengi kutoka ndani na nje ya nchi, wanariadha nyota hapa nchini wakiwemo Fabian Joseph, Dickson Marwa, Mary Naali,Catherine Lange na Jacqueline Sakilu wamethibitisha kushiriki kwenye mbio za km 21 na pia mwaka huu mbio hizo zinatarajia kushirikisha zaidi ya wakimbiaji 800 kutoka nchi 40 duniani.
Baadhi ya nchi ambazo tayari zimethibitisha kushiriki ni pamoja na Marekani, ambayo italeta wakimbiaji wengi zaidi, ikifuatiwa na Uingereza, Canada, Japan, Uganda, Zimbabwe, Kenya, Sweden, Australia na Hungary.
Nchi zingine ambazo zitaleta wakimbiaji wake ni Ujerumani, Sweden, Norway, Italia, Ufaransa, Japan, China, Zambia, Morocco, Swaziland, Nigeria na Malawi.
 Meneja chapa wa Tigo William Mpinga anasema kuwa mbio hizo zinatambulika na Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Riadha (IAAF) na pia zitatumika kufuzu kwa mbio rafiki, ambazo ni zile za Oceans na zingine za kimataifa zilizomo katika kalenda ya IAAF.
Mpinga anasema kuwa wamefurahi kuwa sehemu ya mbio hizo za kila mwaka ambazo zimekuwa na mafanikio makubwa na kuvutia watalii wengi kuja kuona Mlima Kilimanjaro, ambao ni alama na kivutio muhimu cha watalii.
Mpinga alisema mbali na kufurahia mbio hizo za nusu marathoni za Tigo, mashabiki na wakazi wa Moshi mjini watapata fursa ya kuona na kupata bidhaa na huduma za Tigo wakati wa masindano hayo.
 Kama kampuni ya kitanzania pia tunajivunia kushiriki katika tukio hili linalovutia hisia si tu za wanamichezo wengi wa nje, bali pia ni fursa ya kipekee kuonyesha vipaji vya wanamichezo wa ndani, aliongeza.
 UONGOZI WA RT:
Akizungumza hivi karibuni jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania(RT) Suleiman Nyambui anasema kuwa mbio za Kili Marathoni ni mbio kubwa zaidi nchini na maandalizi ya mbio hizo yako katika hatua za mwisho na kusisitiza kuwa zitashirikisha pia nyota wa riadha kutoka nje ya nchi

No comments:

Post a Comment