Wednesday 25 February 2015

MICHEZO KIMATAIFA KWA UFUPI:-




Afcon kuchezwa Novemba 2023


ZURICH, Uswis
KATIBU Mkuu wa Shirikisho la Kimataifa la Soka (Fifa) Jerome Valcke anasema kuwa fainali za Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2023 zitahamishwa kutoka Januari kama ilivyokawaida na kuchezwa Juni, ili kufanikisha fainali za Kombe la Dunia 2022.
Kamati ya Maandalizi ya Fifa imependekeza fainali za Kombe la Dunia zitakaopigwa Qatar zifanyike Novemba na Desemba ili kukwepa joto kali mwezi Juni.
"Kamati ya Shirikisho la Soka la Afrika (Caf) ni wazi itaandaa fainali hizo za Mataifa ya Afrika Novemba na Desemba na sio Januari 2023 kama ilivyozoeleka, alisema Valcke.

***
Serikali yasimamisha ligi Uturuki
 
ATHENS, Ugiriki
SERIKALI ya Ugiriki imesimamisha kwa muda usiojulikana ligi ya kulipwa ya nchi hii kwa sababu ya vurugu, imeelezwa.
Kufungiwa kwa ligi hiyo kumekuja kufuatia vurugu za Jumampili za mchezo wa Super League kati ya Olympiakos na  Panathinaikos, pamoja na ngumi kuzuka miongoni mwa viongozi wa klabu hizo katika mkutano wa bodi Jumanne.
Tayari ligi hiyo msimu huu ilisimamishwa mara mbili katika mwezi Septemba na Novemba.
Kiongozi mpya wa chama cha tawala cha nchi hiyo Syriza ameahidi kukomesha vurugu hizo.

***

Khan awaponda Mayweathe, Pacquiao 

LONDON, England
BONDIA Amir Khan anaamini kuwa pambano la wakali wawili katika ndondi za kulipwa kwa sasa Floyd Mayweather vs Manny Pacquiao litakalofanyika Mei 2, halitakuwa na msisimko.
Bondia huyo Muingereza aliponda kwa kusema kuwa wanamasumbwi hao wawili tayari wakati wao ulikuwa umeshapita, hiyo hawatakuwa na jipya.
Lakini Mayweather anasema kuwa pambano hilo litakalofanyika Las Vegas litakata kiu ya wapenzi wa ndondi duniani.
Pacquiao na Mayweather watakutana Mei 2 baada ya muda mrefu wa makubaliano.

***

Djokovic amsambaratisha  Glubev
 
DUBAI, UAE
MCHEZA tenisi Novak Djokovic alitumia dakika 61 tu kumsambaratisha Andrey Golubev na kutinga robo fainali ya mashindano ya Dubai Duty Free.
Djokovic, ambaye ni bingwa mara nne wa mashindano hayo, kamwe hakumpa nafasi mpinzani wake na kumsambaratisha kwa seti 6-1 6-2 ndani ya saa moja.
Mchezaji tenisi huyo namba moja kwa ubora katika mchezo wa tenisi duniani sasa atapambana na Mturuki Marsel Ilhan, ambaye aliyemshitua anayeshilia nafasi ya sita Feliciano Lopez kwa 3-6 7-5 6-3 aliyeshinda katika kiwanja namba tatu.

No comments:

Post a Comment