Wednesday 11 February 2015

Wavu wa ufukweni watamba kushinda




Kocha Nasoro Sharifu.
Na Mwandishi Wetu
WACHEZAJI wa timu ya taifa ya mpira wa wavu wa ufukweni wametamba kufanya vizuri katika mashindano ya Kanda ya Tano ya Afrika kwa ajili ya kufuzu kucheza Michezo ya Olimpiki itakayofanyika mwakani Rio de Jeneiro, Brazil.
Mashindano hayo ambayo mbali na Tanzania pia yatashirikisha Burundi, Djibout, Somali, Kenya na Ethiopia, yataanza kutimua vumbi Jumatatu Februari 16 hadi 18.
Wakizungumza kwa walisema kuwa wanaendelea vizuri na mazoezi na wana matarajio makubwa ya kufanya vizuri katika mashindano hayo, ambayo yatafanyika kwenye ufukwe wa hoteli ya Mbalamwezi Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Kocha Mkuu wa timu hiyo Nasoro Sharifu alisema kuwa mazoezi yanaendelea vizuri na pamoja na ugeni wa timu ya Tanzania katika mchezo huo, lakini wanatarajia kufanya vizuri sana.


Everline Alberth
Naye mchezaji wa kutumainiwa wa Tanzania Prisons Everlyine Alberth alisema kuwa wana matumaini makubwa ya kufanya vizuri katika mashindano hayo.
Alisema kuwa pamoja na ugeni wa Tanzania katika michuano ya wavu wa ufukweni, lakini watafanya vizuri katika michuano hiyo mikubwa.
Zuhura Jaco wa Jeshi Stars alisema kuwa kuwa wanajiandaa vizuri na lengo lao kuifikisha mbali Tanzania katika mashindano hayo na wanaomba kuungwa mkono na mashabiki.

Zuhura Jaco
Zuhura Jaco wanaendelea vizuri na mazoezi na wana matumaini makubwa ya kufanya vizuri katika mashindano hayo muhimu kwa ajili ya kufuzu kwa Michezo ya Olimpiki.

Hope Agapa.
Naye Hope Agapa alisema wana matumaini makubwa ya kufanya vizuri katika mashindano hayo na lengo lao ni kufika mbali ili kuitoa kimasomaso Tanzania.

Mohamed Ismail.
Mohamed Ismail alisema kuwa mashindano yatakuwa magumu lakini wana matumaini ya kufanya vizuri na kufika mbali.

Farhan Aboubakar au Babu

David Evarist
 
Baadhi ya wachezaji wa timu ya taifa ya wavu wa ufukweni wakipiga msosi jijini Dar es Salaam leo. Timu hiyo inajiandaa kwa michuano ya Kanda ya Tano ya Afrika.
Ford Edward.

No comments:

Post a Comment