Tuesday 3 February 2015

Murray arejea katika nne bora


Murray arejea katika nne bora





LONDON, England
LICHA ya kushindwa na Novak Djkovic katika mchezo wa wikiendi iliyopita wa fainali ya mashindano ya Australian Open, Andy Murray amerejea katika wachezaji wane bora duniani wa mchezo wa tenisi.
Andy Murray amerejea katika nne bora ya viwango vya ubora vya ATP baada ya kutokuwepo kwa miezi 12, akimaliza wa pili katika mashindano ya Australian Open Jumapili.
Mscotland huyo aliporomoka kutoka katika nne bora mwaka mmoja uliopita, huku mara moja tu akifanikiwa kutinga robo fainali ya Melbourne mwaka 2014, lakini amerejea katika nafasi hiyo baada ya kumchapa bingwa namba moja duniani Novak Djokovic na kumyima taji kubwa la tatu katika historia yake ya mchezo huo.
Murray alichapwa 7-6 (7-5) 6-7 (4-7) 6-3 6-0 lakini alirejea katika kiwango chake na kupanda nafasi mbili na kuwa nyuma ya Djokovic, Roger Federer na Rafael Nadal.
Milos Raonic alikuwa mchezaji mwingine aliyeweza kuboresha kiwango chake cha ubora kwa nafasi mbili zaidi, akipaa hadi nafasi ya sita baada ya kutupwa nje na Djokovic katika robo fainali.
Muaustralia Nick Kyrgios alifaidika na mashindano hayo kuchezewa katika ardhi ya nyumbani kwao baada ya kijana huyo mwenye umri wa miaka 19 kupanda hadi nafasi ya 18 kati ya nafasi 35 ikiwa ni mara yake ya pili kucheza robo fainali ya mashindano makubwa.
Mwenzake Bernard Tomic naye amepoteza nafasi ya 18 hadi kuwa wa 48 wakati Stan Wawrinka aliporomoka kwa nafasi tano hadi wa tisa baada ya kushindwa na Djokovic katika hatua ya robo fainali na kumzuia kutetea taji lake.
Kwa upande wa wanawake, Ana Ivanovic aliteleza kutoka nafasi ya tano hadi ya sita baada ya kushindwa na mchezaji kutoka Jamhuri ya Czech Lucie Hradecka katika raundi ya kwanza na Caroline Wozniacki aliyepanda nafasi tatu na kuwemo katika tano bora.
Serena Williams, ambaye hilo ni taji lake la sita la Australian Open lilimsaidia kuendelea kushika usukani huku dada yake Venus alipanda kwa nafasi saba hadi ya 11.

No comments:

Post a Comment