Monday 2 February 2015

Wateja Airtel kuzawadiwa gari kila siku



·Kupitia huduma ya Airtel Yatosha


Watu wakipita mbele ya moja ya magari yatakayotolewa na Airtel Tanzania kwa washindi wa Aiter Yatosha Zaidi.  Add caption

 

Viwanja vya Mlimani City jijini Dar es Salaam vilivyopambwa wakati wa uzinduzi wa Airtel Yatosha Zaidi leo

Mpanda pikipiki akifanya manjonjo wakati wa uzinduzi wa shindano la Airtel Yatosha Zaidi jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya magari yatakayoshindanishwa kwa wateja wa Airtel watakaoshiriki shindano la Airtel Yatosha Zaidi wakati wa uzinduzi wa shindano hilo leo katika viwanja vya Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Gari aina ya Toyota IST likionekana kwa nyuma wakati wa uzinduzi wa shindano la Airtel Yatosha Zaidi.
Mpanda baiskeli akifanya vitu vyake wakati wa uzinduzi wa shindano la Airtel Yatosha Zaidi. Pembeni ni magari aina ya Toyota IST yatakayoshindaniwa na wateja wa wanaotumia mtandao wa Airtel Tanzania. (Picha Zote na Cosmas Mlekani).
Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Simu za Mkononi ya Airtel Tanzania, leo imezindua promosheni  kabambe ijulikanayo kama Airtel Yatosha Zaidi kwa wateja wanaotumia vifurushi vya Airtel Yatosha kuweza kujishindia gari aina ya Toyota IST kila siku.


Akiongea wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo Mkurugenzi wa Masoko ya Airtel Bwana Levi Nyakundi alisema promosheni hiyo ni nafasi ya kipekee kwa wateja wanaojiunga na vifurushi vya Airtel yatosha vya siku, wiki na mwezi kupata faida zaidi kutokana pesa wanazozitumia. 

Alisema kuwa wateja hao watapata zawadi nono kibao kila siku ikiwemo gari la aina ya Toyota IST.

Nia yetu  kuhakikisha tunatoa huduma na bidhaa bora kwa kupitia huduma yetu ya Airtel Yatosha, huku tukiwazawadia wateja wetu zawadi nono, alisema na kuongeza:
Tunaamini promosheni hii itawapatia wateja wetu uzoefu tofauti wakati wote wakitumia huduma zetu za Airtel Yatosha. Zaidi ya wateja wetu kijishindia magari promosheni hii ya Airtel Yatosha Zaidi itawapatia wateja wetu vifurushi zaidi,” aliongeza Nyakundi

Akiongea kuhusu namna ya kushiriki Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi. Beatrice Singano Mallya alisema ili kushiriki kwenye promosheni hii wateja wanatakiwa kuendelea kununua vifurushi vyao vya Yatosha vya siku, wiki na mwenzi.

Alisema hakuna gharama ya ziada, kwa kununua vifurushi vya yatosha tayari utakuwa umeunganishwa kwenye droo ya yatosha zaidi na kupata nafasi ya kujishinidia Toyota IST moja kila siku

Hii ni promosheni ya aina yake ambapo wateja wetu wanazawadiwa kutokana na matumizi yao ya kawaida ya vifurushi vya Yatosha.  tunatoa wito kwa wale ambao hawajajiunga na vifurushi vya Airtel yatosha kufanya hivi na kupata nafasi ya kushinda gari moja kila sikualiongeza  Mallya

Kununua vifurushi vya yatosha wateja wanaweza au  kupiga *149*99#, kunua kwa kupitia huduma ya Airtel Money au kwa kununua vocha ya Airtel yatosha inayopatikana katika maduka yetu nchi nzima

Mwaka Jana Airtel ilizindua huduma ya kisasa ya kibunifu na yenye vifurushi vya gharama nafuu sokoni. Kuzinduliwa kwa promosheni hii ya Airtel yatosha Zaidi ni mwendelezo wa dhamira ya Airtel ya kutoa huduma bora huku ikiwazawadia wateja wake kwa kutumia huduma zake

Mwisho

No comments:

Post a Comment