Tuesday 10 February 2015

Jamhuri aipandisha Mwadui ya Shinyanga




Kocha Mkuu wa Mwadui Jamhuri Kihwelo akisisitiza jambo.

Na Mwandishi Wetu
HATIMAYE timu ya Mwadui FC ya Shinyanga imepanda daraja na msimu ujao itashiriki Ligi Kuu Tanzania Bara, imeelezwa.
Timu hiyo ambayo mwaka jana nusura icheze Ligi Kuu kama sio kufanyiwa mizengwe, inafundishwa na kocha wazamani wa Simba Jamhuri Kihwelo.
Kupanda kwa Mwadui ni faraja kubwa kwa viongozi wa soka a mkoa wa Shinyanga kwani sasa mbali na timu hiyo pia kuna timu ya Stand United ambao wanashiriki Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mwandui imepanda daraja baada ya kujihakikishia pointi 43 baada ya kuikandika Polisi ya Tabora kwa bao 2-0 katika mchezo uliopigwa mkoani Shinyanga.
Aidha, mchezo mwingine wa kundi B kati ya Toto African ya Mwanza na Geita Gold SC ulivunjika baada ya kutokea vurugu na mwamuzi kupokea kichampo.
Toto African ya Mwanza wana pointi 39 wakiwa mbele ya JKT Oljoro pamoja na Polisi Tabora ambao kila mmoja ana pointi 38.
Mwaka jana Julio alitaka kuipandisha timu hiyo Ligi Kuu lakini kufuatia TFF kuchelewa kutoa maamuzi baada ya mchezo wao na Stand United kuvunjika na kusababisha kutotinga Ligi Kuu na badala yake msimu huu kucheza Ligi Daraja la kwanza.






No comments:

Post a Comment