Tuesday 24 February 2015

Serikali ya Kenya yapata pigo kubwa




*Mahakama yapunguza vipengele vya sheria ya ugaidi


Kenyatta International Conference Centre (KICC).
Nairobi, Kenya
SERIKALI ya Kenya imepata pigo baada ya Mahakama ya Katiba kuondoa baadhi ya vipengele katika sheria mpya ya usalama ili kukabiliana na ugaidi.
Muungano wa upinzani nchini Kenya na mashirika mbalimbali yalienda mahakamani mwaka uliopita baada ya bunge kupitisha sheria hiyo.
Jopo la majaji watano wa Mahakama Kuu wakiongozwa na Jaji Isaac Lenaola walifutia mbali vipengele 10 kikiwemo kile kinachohusu uhuru wa vyombo vya habari na haki ya washukiwa wanapofikishwa mahakamani.
Uamuzi huo ulichukua kama saa saa tano na majaji wakaamua kuwa baadhi ya vipengele havikuaambatana na Katiba.
Katika uamuzi wao walikubali kuwa Kenya imekumbwa na visa vingi vya ugaidi katika miaka ya hivi karibuni na inastahili kuwa na mbinu za kuisaidia kukabilana na tatizo hilo.
Majaji hao walisema kuwa haki ya washitakiwa inatakiwa kuzingatiwa pia.
Mengine yaliyoharamishwa yanajumuisha kuwalazimisha wanahabari kuchapisha baadhi ya picha kwa ruhusa ya polisi,
kuwazuia washukiwa bila kuwapa nafasi ya kujitetea na kuwanyima dhamana washukiwa wakipelekwa mahakamani bila sababu zozote.
Aidha, mahakama hiyo imekataa jaribio la Serikali kutaka kuweka kiwango cha wakimbizi wanaostahili kuhifadhiwa Kenya wazidi 150,000 na kusema hiyi ni kinyume na mkataba Geneva.
Uamuzi huo wa mahakama umefueahia na Muungano wa upinzani wa CORD.
Hatahivyo, serikali kupitia wakili wake imesema kuwa iko njiani kukataa rufaa k,upinga uamuzi huo wa mahakama.
Sheria hiyo ilipitishwa Bungeni Desemba 14 mwaka jana katika kikao kilichotawaliwa na vurugu huku baadhi ya wabunge wakizichapa kavu kavu.

No comments:

Post a Comment