Monday 9 February 2015

Ukata waahirisha ndondi za mchujo BFT





Na Mwandishi Wetu
MASHINDANO ya mchujo ya ndondi za ridhaa yaliyopangwa kuanza leo Jumatatu kwenye Uwaja wa Ndani wa Taifa jijini Dar es Salaam, yameahirishwa, imeelezwa.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Ndondi Tanzania (BFT) Makoye Mashaga alisema kuwa ukosefu wa fedha ndio umewafanya kuyasogeza mbele mashindano hayo.
Aliwataka wadau mbalimbali wa michezo na ndondi kujitokeza kusaidia kudhamini mashindano hayo ili kuhakikisha yanafanyika kwa ufanisi mkubwa ilikupata timu bora ya taifa.
Alisema mashindano hayo yatashirikisha jumla ya mabondia 39 lakini watachujwa na kubaki 15 tu ambao wataingia kambini kwa ajili ya kujiandaa kwa michezo hiyo ya Afrika itakayofanyika Brazzaville, Kongo Septemba mwaka huu.

MABONDIA AMBAO WATASHIRIKI MCHUJO HUO:-
Lightfly: Ibrahim Abdallah (Magereza), Said Hofu (JKT), Gervas Longasian (Arusha), Said Stephen (Kigoma).
Fly: Shabani Mnimba (Temeke), Hafidh Mohamed (JKT), Muhsin Kimwaga (JKT), Michael Andrew (Temeke).
Bantam: Tuwer Son (JKT), James Star (JKT), Ahmed Furahisha (JKT), Bashir Mkumbula (JKT), Robert Nobert (Kagera), Hassan Yussuf (Magereza).
Light: Bosco Bakari (JKT), Swahiba Athumani (Arusha), Mohamed Ibrahim (Tanga) na Undule Langson (Magereza), Fidel Castro (Kigoma) na Silaji Kassim (Kagera).
Walter: Victor Njaiti (JKT), Issa Rashid (JKT), Shaban Bruno (Arusha), Kassim Khalfan (JKT) na Babu Buluda (Morogoro).
Lightmiddle: Gulash Rashid (JKT), Seleman Bamtula (JKT) na Mustapha Mtoro (Temeke).
Middle: Ivan Mussa (Kagera), Abuu Said (JKT), Hafidh Mwaipaja (Magereza), Frank Florian (Kigoma).
Lightheavy: Robert Kyaruz (Kagera), Frank Kawesi (Lindi), Freddy Julius (Kigoma) na Daniel Mwambinga (Magereza).
Heavy: Alex Sitta, Maulid Kitenge na Fabian Gaudence.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment