Monday 9 February 2015

Yaya Toure apagawa na ubingwa Afrika



 *Aamini kama wameitoa Ghana kwa penati 9-8 katika fainali



Nahodha wa Ivory Coast Yaya Toure baada ya kukabidhiwa Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kuifunga Ghana kwa penati
MALABA, Guinea ya Ikweta
KIUNGO wa Ivory Coast na Manchester City Yaya Toure anaelezea kushinda taji la Mataifa ya Afrika kama ni `kitu asichoamini baada ya Tembo kuwafunga Ghana `The Black Stars kwa mikwaju ya penati.
Kipa Boubacar Barry alifunga penati muhimu na kuifanya Ivory Coast kushinda kwa penati 9-8 baada ya mchezo huo wa fainali kumalizika kwa suluhu katika dakika 120.
Toure, aliyeshinda taji la Ligi Kuu ya England akiwa na Manchester City msimu uliopita, alisema: "Unaposhinda ukiwa na kalbu yako, ni furaha ya aina yake.
"Unapotwaa taji na nchi yako, ni kitu ambacho sikukitarajia."
Ivory Coast ilipata mafanikio pekee mwaka 1992, wakati ilipotwaa taji hilo walipocheza tena na Ghana katika fainali na kuwafunga tena kwa penati.
Mwaka huo, Ivory Coast ilishinda kwa penati 11-10 baada ya sare ya kutofungana, lakini Barry aliokoa penati kibao wakati uo.
Wakati wa kupigiana penati, Barry kwanza aliokoa mchomo wa penati uliopigwa na kipa mwenzake Brimah Razak kabla hajafunga penati ya ushindi katika mchezo huo wa fainali uliopigwa kwenye uwanja wa Bata nchini Guinea ya Ikweta.
Naye kocha wa timu hiyo Herve Renard aliweka historia, baada ya kuwa kocha wa kwanza kutwaa mara mbili taji la Mataifa ya Afrika akiwa na nchi mbili tofauti, kufuatia kutwaa taji na Zambia mwaka 2012.

"Bila kocha tusingeshinda taji, " aliongeza Toure, ambaye ni nahodha wa Ivory Coast.
Kushindwa kwa Ghana kocha Avram Grant kunamkumbusha mwaka 2008 wakati wa mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya Chelsea ilipotolewa kwa penati 6-5 na Manchester United, huku John Terry akiteleza na mpira wake kugonga mwamba alipopiga mpira.

No comments:

Post a Comment