Sunday 8 February 2015

Uchaguzi Mkuu Nigeria waaihirishwa



 *Ni hofu ya Boko Haramu

LAGOS, Nigeria
NIGERIA imeahirisha kwa wiki sita uchaguzi wake mkuu wa rais uliopangwa kufanyika Jumamosi kwa sababu ya hofu ya kiusalama. Imeelezwa.
Kiongozi wa Kamisheni ya Uchaguzi ya Nigeria Attahiru Jega (pichani) alisema uchaguzi huo mkuu umeahirishwa hadi Machi 28 na ilikuwa muhimu kufanya hivyo kwa sababu ya kutokuwepo kwa vikosi vya ulinzi vya kutosha kwa ajili ya kuwalinda wapiga kura.
Jeshi la Nigeria limekuwa likipigana na wapiganaji wa Boko Haram huko kaskazini-mashariki ya nchi.
Hatahivyo, vyama vya upinzani vimesema kuwa kitendo hcho cha kuahirisha kwa uchagui huo ni kurudisha nyuma demokrasia ya Nigeria.
Kiongozi wazamani wa kijeshi Muhammadu Buhari, kutoka chama cha All Progressives Congress (APC) anapambana na rais aliyemadarakani Goodluck Jonathan, anayeongoza chama cha People's Democratic Party (PDP).
Habari zinasema kuwa hadi uchaguzi huo unaahirishwa mchuano ulikuwa mkali kati ya viongozi hao wawili.
Bwana Jega jana Jumamosi alitangaza kuahirishwa kwa uchaguzi huo.
Alisema kuwa hatua aliyoichukua ni muhimu kwani alieleza kuwa vikosi vya usalama havitakuwepo kusaidia wakati huo wa uchaguzi kwani viko katika zoezi maalum la kupambana na wapiganaji wa Boko Haram.
"Kamishemi ya uchaguzi kamwe haiwezi kupuuza ushauri wa kiongozi wa usalama wa nchi, " alisema bwana Jega.
"Kuwaita watu kutekeleza haki yao ya kidemokrasia katika hali isiyo ya kiusalama ni suala lisilofaa kabisa.
Hatahivyo, viongozi kutoka APC wamelaani hatua hiyo ya kusogeza mbele uchaguzi huo wakidai kuwa hatua hiyo ni kutaka kusaidia kampeni za rais aliyopo madarakani.
Mwenyekiti wa APC John Odigie-Oyegun alisema kitendo hicho cha kuahirisha uchagui huo ni pigo kubwa kwa demokrasia ya Nigeria ".

No comments:

Post a Comment