Tuesday 24 February 2015

Andy Murray aanza vizuri Dubai Open




Andy Murray akirudisha mpira katika mashindano ya Dubai.
LONDON, England
MUINGEREZA Andy Murray ameanza vizuri kampeni zake za kutwaa ubingwa wa mashindano ya Dubai baada ya kuibuka na ushindi wa seti 6-4 7-5 dhidi ya Gilles Muller.
Mscotland huyo, mwenye umri wa miaka 27, alipata ushindi huo kwa kutumia saa moja na dakika 45, na sasa atacheza na Joao Sousa katika raundi ya pili, ikiwa ni wiki mbili baada ya kumshinda Mreno huyo katika mashindano ya Australian Open.
Bingwa anayeongoza kwa ubora Novak Djokovic naye alianza vizuri mashindano hayo baada ya ku
mchakaza Mcanada Vasek Pospisil 6-4 6-4 katika mchezo wa rundi ya kwanza.
James Ward ambaye ni Muingereza anayeshikilia nafasi ya pili kwa ubora, alijikuta akishindwa kufanya kweli baada ya kushindwa mara mbili katika hatua ya kufuzu na kupoteza kwa 6-4 6-4 dhidi ya Muhispania Feliciano Lopez, anayeshikilia nafasi ya 13 kwa ubora duniani.
Muingereza huyo sasa atakwenda Glasgow kujiunga na timu ya Uingereza itakayocheza mchezo wa Davis Cup dhidi Marekani, utakaofanyika kuanzia Machi 6-8 huko Emirates.
Murray anatarajia kukawia kujiunga na wenzake huko Scotland endapo ataendelea kufanya vizuri huko Dubai baada ya leo kuanza vibaya mchezo huo katika jaribio lake la kwanza, lakini alifanya vizuri na kuibuka na ushindi katika seti hiyo ya kwanza.
Djokovic anashiriki kwa mara ya kwanza tangu alipotwaa taji la Australian Open Februari mosi na anaangalia kuwa mtu pekee wa 12 kushinda taji la 50.

No comments:

Post a Comment