Thursday 26 February 2015

Boko Haram waendelea kuua Nigeria




ABUJA, Nigeria
SHAMBULIZI la bomu limeaua watu 32 Kaskazini ya Nigeria, ikiwa ni muendelezo wa matukio ya kundi la Boko Haram.
Imeelezwa kuwa bomu katika kituo cha basi cha Biu limeua kama watu 17, amesema shuhuda mmoja, wakati lile la pili linaelezwa kuwa liliua watu kadhaa.
Huko Jos, mabomu matatu yalitupwa kutoka ndani ya gari na yaliua watu 15 katika kituo cha basi na emeo la Chuo Kikuu.
Uchaguzi wa rais uliopangwa kufanyika mwezi huu, uliahirishwa kutokana vurugu hizo za Boko Haram.
Uchaguzi huo sasa unatarajia kufanyika Machi 28 mwaka huu.
Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan, aliyetembelea mji huo wa kaskazini-mashariki wa Baga, alisisitiza kuwa, jeshi la serikali limeshinda vita dhidi ya Boko Haram.
Jeshi la serikali wiki iliyopita liliurejesha mji wa Baga uliokuwa ukishikiliwa na Boko Haram. Kundi hilo bado linashikilia sehemu kubwa ya kaskani-mashariki ya Borno na zaidi ya watu milioni tatu wamekimbia nyumba zao.
Mashambulizi huko Kano na Potiskum Jumanne yamechukua maisha ya watu zaidi ya 50. Hakuna kundi lililojitokeza na kusema kuwa limehusika namashambulizi hayo.

No comments:

Post a Comment