Wednesday 4 February 2015

Ghana wataka kipa wa Guinea afungiwe





MALABA, Equatorial Guinea
KOCHA wa timu ya taifa ya Ghana ya Black Stars Avram Grant (pichani) analitaka Shirikisho la Soka la Afrika kumfungia kipa wa Guinea Naby Yattara.

Kipa huyo anayecheza soka Ufaransa alipewa onyo Jumapili katika mchezo war obo fainali wa Mataifa ya Afrika (Afcon) walipocheza na Ghana wakati alipomrukia mshambuliaji Asamoah Gyan katika kipindi cha mwisho kabisa cha mchezo huo.

"Wakati matokeo yakiwa ni 3-0 na tulikuwa katika dakika za mwisho kabisa za mchezo, faulo ile ilionesha kutokuwa na nidhamu. Sifikiri kama atacheza soka tena kwa sabbau kama unataka kuwaondoa mchezoni wachezaji, watu wanatakiwa kufikiriakuhusu hilo

"Nafikiri anatakiwa kufungiwa maisha yote. Hatakiwi kucheza soka kwa sababu alijaribu kumuumisha Mghana Gyan. Alifanya kosa lile kwa makusudi kabisa katika neo la tumbo la mwenzake."

Kocha huyo Muisraeli alifananisha faulo hiyo na ile iliyofanywa na kipa wa Ujerumani Holord `Toni Schumacher alipomchezea vibaya mchezaji wa Ufaransa Patrick Battison.

"lakini hii ni mbaya zaidi, " alisema Grant aliyewahi kuwa kocha wa Chelsea ya England.

Gyan alipandishwa ndege kwenda Mongomo Kaskazini ya Equatorial Guinea kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya scan wakati Ghana ilipoanza mazoezi jijini Malabo bila ya nahodha wao huo kwa ajili ya kuwakabiri wenyeji katika mchezo wa nusu fainali kesho.

No comments:

Post a Comment