Thursday 5 February 2015

Moyes aliwazuia Man United kula vyepe



MADRID, Hispania
KOCHA wazamani wa Manchester United David Moyes amekiri kuwa, alipiga marufuku wachezaji wake kula chips wakati akifundisha klabu hiyo yenye maskani yake Old Trafford.
David Moyes alisema kuwa alizuia wachezaji wake kula chips kwa sababu alihisi baadhi yao waliongezeka uzito kutokana na kupenda kula chakula hicho.
Moyes alikosolewa kufuatia kutimuliwa kwake Aprili mwaka jana, huku Rio Ferdinand ambaye ni beki wa kati wazamani wa Man United akikosoa uamuzi wa kocha huyo Mscotland wa kuzuia msosi huo kwa wachezaji wa timu hiyo.
Ulaji wa chips ulikuwa wa kawaida sana wakati wa kipindi cha kocha Alex Ferguson aliyemtangulia Moyes hapo Manchester.
Moyes kwa sasa anafundisha timu inayoshiriki Ligi Kuu ya Hispania ya La Liga ya Real Sociedad alifunguka kuhusu sababu za kupiga marufuku ulaji wa chips alipokuwa Manchester United.
Kocha huyo alidai katika mahojiano na gazeti la Four Four Two kuwa, baadhi ya wachezaji walikuwa vibonge.
Ndio, nilizuia ulaji wa chips," alisema Moyes, ambaye alifundisha kwa miezi sita tu katika mkataba wake wa miaka sita pale Man United.
"Kwa sababu wachezaji baadhi ya wachezaji walikuwa vibonge na sikufikiri kama chips ulikuwa mlo mzuri kwao."
Moyes pia alikiri kuwa hakufurahishwa na mapokezi aliyapata wakati Man United waliposafiri kwenda Goodison Park katika msimu wa mwaka 2013-14.
Baada ya miaka 11 ya kuifundisha Everton, Moyes alirejea na kupokewa kwa kuzomewa huko Merseyside wakati Man United ikichapwa 2-0 dhidi ya klabu yake hiyo ya zamani.
Moyes, aliyetimuliwa baada ya kipigo hicho, alisema: "Sikushtushwa, kwa sababu najua jinsi mashabiki walivyo na niliwaachia klabu yao. Lakini nilisikitika sana kwa kitendo kile.
    

No comments:

Post a Comment