Saturday 28 February 2015

Buriani Kapteni John Damiani Komba





Kapteni John Damiani Komba
Na Mwandishi Wetu

MBUNGE wa Mbinga Magharibi na Mkurugenzi wa kundi la The Tanzania One Theatre (TOT) Kapteni John Komba amefariki funia leo hii.
Habari zilizotufikia na kuthibitishwa na Katibu Mipango wa TOT Plus Gasper Tumaini zinasema kuwa, Komba amefariki leo Jumamosi jijini katika hospitali ya TMJ Mikocheni, ambako alikimbizwa baada ya kuzidiwa na kisukari akiwa nyumbani kwake Mbezi Beachi eneo la Tangi Bovu jijini Dar es Salaam.
Imeelezwa kuwa mbunge huyo alifariki hospitalini hapo wakati akipatiwa matibabu.
Mbunge huyo alizidiwa akiwa nyumbani kwake Mbezi na kukimbizwa hospitalini hapo akisumbuliwa na ugonjwa wa Kisukari.
Tumaini alithibitisha kuwa Komba alifariki dunia hospitalini na alikuwa hana mengi ya kusema kwani wakati huo akizungumza na mwandishi wa habari hizi walikuwa nyumbani kwa Komba wakiendelea na taratibu zingne.
Ni kweli amefariki na sasa tuko kwake tunaendelea na taratibu zingine na taarifa zaidi zitatolewa kesho (Jumapili), alisema Tumaini kwa kifupi.
Bwana Alitoa na Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe, Amina.

No comments:

Post a Comment