Sunday 8 February 2015

Sare yamchanganya Manuel Pellegrini




Kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini
LONDON, England
KOCHA wa Manchester City Manuel Pellegrini amekiri kuwa kikosi chake lazima kijiimarishe zaidi baada ya kutoka sare ya 1-1 na Hull City katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.
Mabingwa hao wa Ligi Kuu walihitaji bao la dakika za mwisho lililotokana na mpira wa adhabu uliopigwa na James Milner na kuzuia timu hiyo kupata kipigo cha tatu mfululizo baada ya David Meyler kuifungia Hull bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza.
Hatahivyo, City, sasa wana pointi saba nyuma ya Chelsea, ambapo sasa inakabiliwa na kibarua kigumu kutetea taji lake hiyo na imeshinda moja kati ya mechi sita za Ligi Kuu, huku vinara wa ligi wakishinda 2-1 huko Aston Villa na kujiimarisha uongozi wao kileleni.
“Lazima kujiimarisha zaidi kwa sababu timu inacheza na wachezaji 10 na pamoja na yote hatukutengeneza nafasi wala kufunga, ” alisema Pellegrini. Kila pointi unayopoteza ni ngumu kuipata; kurejesha pointi saba ni ngumu sana zaidi ya tano lakini huwezi kujua.
“Kwa kweli hatufikirii kabisa kuhusu Chelsea, wanaoongoza kwa pointi saba katika msimamo wa ligi lakini nao pia wanaweza kupoteza mchezo. Muhimu zaidi kwetu ni kuimrisha safu yetu ya ushambuliaji.
Mabingwa hao watetezi walijitahidi wakitoana jasho na Hull City wakati wakishindwa kuibuka na ushindi kwa mara ya tano katika mashindano yote.
“Tulimiliki mpira zaidi. Tulifanya kazi ya ziada, tulikimbia, na kuchukua mipira, lakini inahitaji mipango unapocheza na timu kama Hull, Middlesbrough au Arsenal ambao watakuja hapa na wachezaji tisa au 10 nyuma ya mpira, alisema Pellegrini.
“Inachanganya kwa sababu timu ilifanya kazi wakati wote wa mchezo. Tulicheza zaidi, tulifanya kila siku na tulifanya kila kitu…, “ alisema.
Man City itaongezewa nguvu na kurejea kwa Wilfried Bony na Yaya Toure baada ya kumalizika kwa fainali za Mataifa ya Afrika wiki hii lakini Pellegrini aligoma kukilaumu kikosi chake kwa kukosekana wachezaji hao.
“Watasaidia wakiwepo lakini zaidi ya kuwafirikia wao kinachotakiwa ni kufikiria wachezaji wanaocheza kwa sasa, ” aliongeza kocha huyo.
“Labda inatubidi kutafuta njia nyingine ya kucheza. Ni vigumu kujua sababu moja ya kutofanya vizuri.”


No comments:

Post a Comment