Saturday 21 February 2015

Kauli ya Rais wa IAAF yapingwa vikali



 
Bingwa wa Olimpiki Christine Ohuruogu.
LONDON, England

BINGWA wa Olimpiki Christine Ohuruogu amekosoa kauli ya rais wa Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Riadha (IAAF) kuwa, mchezo wa riadha unakabiliwa na mgogoro mkubwa dhidi ya matumizi ya dawa za kuongeza nguvu.
Rais huyo wa IAAF Lamine Diack alisema kuwa "alishtushwa" na madai kuwa viongozi wa IAAF walitumika kulinda matumizi ya dawa hizo nchini Russia.
"Ni viguu sana kuendeleza mchezo wetu wakati hajui kinachoendelea, " alisema Ohuruogu.
Akizungumza BBC radio 5 Live, Ohuruogu alisema: "Nafikiri aina hiyo ya kauli haitakiwi…”
Desemba, TV ya Ujerumani ilidai kuwa viongozi wa riadha wa Russia walikubali malipo kutoka kwa wanariadha kugawa dawa hizo zilizopigwa marufuku na kuzuia usifanyike upimaji.
Wote waliodaiwa sasa wanachunguzwa na Kamishenu ya Nidhami ya IAAF, ambayo itaamua kama viongozi wa kamisheni ya Russia ya kuzuia matumizi ya dawa hizo, walihusika katika hilo.
Lakini Diack, ambaye atamaliza muda wake wa uongozi Agosti mwaka huu baada ya kukalia kiti hicho kwa takribani miaka 16 kama mtu mwenye nguvu sana katika mchezo huo, alikanusha kama kuna mtu yeyote anayelindwa.
Kwa mara ya kwanza akifanya mahojiano hadharani katika vyombo vya habari tangu kutolewa kwa tuhuma hizo, Diack alisema: "Ni mgogo mgumu lakini tutauweka kando na kusafisha hali hii ya hewa."
Ohuruogu alifungiwa kukimbia kwa mwaka mmoja baada ya kushindwa katika vipimo mara tatu kabla hajarejea na kutwaa medali ya dhahabu.
Pia mdada huyo alishinda medali ya Olimpiki yam bio za mita 400 katika Olimpiki ya Beijing meaka 2008 na kuwa Muingereza wa kwanza mwanamke kushinda mara mbili katika mashindano ya dunia wakati alipotwaa dhahabu huko Moscow mwaka 2013 na kuongeza katika taji lake la mwaka 2007.

No comments:

Post a Comment