Wednesday 11 February 2015

Rais Ivory Coast amwaga mapesa



 *Kila mchezaji apata pesa na mjengo wa nguvu


Rais wa Ivory Coast, Alassane Ouattara na nahodha Yaya Toure.
YAMOUSSOUKRO, Ivory Coast
RAIS wa Ivory Coast Alassane Ouattara jana alimwaga mapesa zaidi ya dola za Marekani Milioni 3.4 ikiwa ni zawadi kwa timu ya taifa ya nchi hiyo kutwaa taji la Mataifa ya Afrika.
Waziri wa Michezo alisema kuwa rais amefurahishwa sana na ushindi wa timu hiyo na ndio maana akatoa kiasi hicho cha fedha.
Timu hiyo kutoka Afrika Magharibi iliifunga Ghana kwa penati 9-8 vbaada ya timu hizo kutoka suluhu katika muda wa kawaida na ule wa nyongeza katika fainali huko Guinea ya Ikweta.
Hilo ni taji lao la pili la Afrika kulitwaa baada ya lile la mara ya kwanza mwaka 1992.
Kocha Herve Renard alikaribishwa katika makazi ya rais jana na Mfaransa huyo alipata bonasi ya dola za Marekani 129,000.
Kikosi chake cha wachezaji 23 kila mmoja alipewa nyumba yenye thamani ya 52,000 pamoja na fedha taslimu zenye thamani hiyo, kwa mujibu wa waziri wa michezo Alain Lobognon.
Shirikisho la Soka la Ivory Coast lilipewa kiasi cha dola za Marekani 429 000, pamoja na benchi la ufundi waligawana kiasi cha dola 520 000, na kufanya fedha zilizotolewa na rais kuwa ya jumla ya pauni Milioni 3.

"Ahsanteni sana, kwa mara nyingine tena Ivory Coast imeungana tena, " alisema Ouattara.
Umati wa watu ulifurika katika uwanja wa Felix Houphouet-Boigny jijini Abidjan, ambako wachezaji waliingia katika gari la wazi pamoja na rais wa nchi hiyo.

Umati wa wananchi wa Ivory Coast ukisubiri timu yao.

No comments:

Post a Comment