Monday 16 April 2018

TAA Kukusanya Bilioni 134, Waanzisha Tozo Mpya

Waziri wa Uchukuzi na Mawasiano, Makame Mbarawa akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) jijini Dar es Salaam leo.

Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) inatarajia kukusanya kiasi cha Sh bilioni 134 kupitia viwanja vyake kwa mwaka wa fedha 2018-19, imeelezwa.

Pia Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Richard Mayongela amesema leo kuwa mamlaka yake iko mbioni kuanzisha tozo mpya ya usalama, ambayo huko nyuma haikuwepo na inatarajia kuwaongezea mapato.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Rochard Mayongela akizungumza baada ya uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi wa TAA.
Mayongela alisema kuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukizi, Profesa Makame Mbarawa ameridhia kuanzishwa kwa tozo hiyo ya usalama, ambayo watatozwa abiria wanaondoka kupitia viwanja vya ndege hapa nchini.

Hayo yamesemwa leo na Mayongela, ambaye ni mwenyekiti wa baraza hilo la wafanyakazi la TAA, ambalo ni la 21 wakati likizinduliwa leo katika jengo la NSSF Ilala Jijini Dar es Salaam.
Anasema Waziri ameridhia kuanzishwa kwa tozo hiyo ya usalama kutokana na changamoto zilizopo za kiusalama katika viwanja vyetu vya ndege.

Alimshukuru Waziri kwa kufika licha ya majukumu mengi aliyonayo katika kpindi hiki cha Bunge la Bajeti kinachoendelea mjini Dodoma, ambapo alisema kuwa wafanyakazi wanataka kusikia maslahi yao yanaboreshwa.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) wakati wa uzinduzi wa baraza hilo leo.
Mbarawa aliwapongeza wafanyaakzi wote waliochaguliwa kuwa wajumbe wa baraza hilo na kuwaambia kuwa kazi ndio kwanza inaanza na wao ndio injini na ndio wanaangalia maslahi ya wafanyakazi, kwani wao ndio kiungo kati ya wafanyakazi na uongozi.

Alisema Serikali inawathamini sana na wako pale kisheria na aliwataka kushirikiana na serikali, ambapo pia aliwakumbusha majukumu yao baada ya kuchaguliwa.
Alitaka wajumbe wa baraza hilo kujiuliza wamewafanyoia nini wadau wa viwanja vya ndege na wamewafanyia nini Watanzania na kupanga bajeti vizuri na kama hawajafikia amewataka kuhoji sababu za kutofikia bajeji ya mwaka 2017-18 na kama wamefikia malengo wajipongeze.

Pia amewataka kujiuliza sababu za viwanja vya ndege Tanzania Bara kutokuwemo katika orodha ya viwanja 10 bora vya ndege barani Afrika, wakati Zanzibar kimo katika viwanja bora.
Alihoji sababu za TAA kushindwa hata kununua gari la zima moto na badala yake kusubiri fedha kutoka Serikali Kuu wakati wana vyanzo vingi vya mapato, ambavyo kama wangevitumia vizuri wangeweza kujinuliwa wenywe magari hayo.

Alisema Watanzania na wasafiri wengi bado wana imani na viwanja vya ndege vya Tanzania, lakini tatizo ni kasoro ndogo ndogo ndizo zinafanya tushindwe kuwa miongoni mwa viwanja bora barani Afrika.

Alisema kama hatuko katika viwanja bora huo ndio mwanzo wa kupoteza watalii kwani wengi watakimbilia Kenya ambako kuna viwanja bora kuliko sisi na wakipungua, basi wafanyakazi wengine watapunguzwa.

Aliwataka kufanyakazi kwa bidii ili kujiongezea mapato na kubuni miradi mingine, ambayo itawawezesha kupata fedha, na alimpngeza Mayongela kwa kuwa nampango wa kununia magari sita kwa mpigo, kitu ambacho huko nyuma hakijawahi kufanywa.

No comments:

Post a Comment