Friday 14 April 2017

VURUGU ZA MASHABIKI ZACHELEWESHA KUANZA PAMBANO LA LYON NA Besiktas

LYON, Ufaransa
VURUGU jukwaani zilisababisha baadhi ya mashabiki kukimbilia sehemu ya kuchezea na kuchelewesha kuanza kwa mchezo wa kwanza wa robo fainali wa Ligi ya Ulaya kati ya Lyon na Besiktas.

Hatahivyo, wenyeji ndio walikuja kuibuka na ushindi wa bao 2-1 katika mchezo huo.
Vurugu zilitokea na kusababisha polisi kuingilia kati nje ya uwanja kabla ya kuibukia nyuma ya goli ambako wachezaji walikuwa wakipasha.

"Vitu ukiwemo moto vilirushwa kutoka jukwaani nakusababisha baadhi ya wapenzi kuwa wakimbizi kwa muda uwanjani ili kuokoa maisha yao, “ Lyon walitweete.

Mchezo huo ulianza baada ya dakika 45 huku Lyon ikifunga mara mbili katika dakika 10 za mwisho nan aibuka na ushindi wa mabao 2-1.


Mamlaka walitenaga maeneo yenye riski kubwa, ambapo askari 500 walimwagwa kwenye Uwanja wa Parc Olympique Lyonnais ikiwa ni zaidi ya idadi ya kawaida.

No comments:

Post a Comment