Saturday 7 April 2018

Ngorongoro Marathon; Mbio za Kukimbiza Jangili


Na Mwandishi Wetu
MBIO za Ngorongoro Marahon zenye lengo la Kukimbiza Jangili, ambazo mwaka huu zitafanyika Aprili 21 zimefikia katika hatua nzuri.

Kauli Mbiu yam bio hizo mwaka huu ni `Kukimbiza Jangili’, ambapo Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCCA) ndio mdhamini mkuu ikisaidia na Bonite Bottlers ya mjini Moshi, ambayo hutengeneza maji ya Kilimanjaro na soda jamii ya Coca Cola.

Tayari wanariadha zaidi ya 200 wamejisajili kwa ajili ya kushiriki mbio hizo, ambazo waandaaji wanasema kuwa mwaka huu zitakuwa na msisimko mkubwa katika maeneo tofauti tofauti.

WAANDAAJI WANENA
Mkurugenzi wa mbio hizo, Meta Petro akizungumza na gazeti hili anasema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na ni matarajio yao makubwa kuwa mwaka huu msisimko utakuwa mkubwa zaidi tofauti na mwaka jana.

Alisema kuwa ni mataraji yao kuwa mwaka hadi mwaka mashindano hayo yatakuwa yakibadilika na kushirikisha washiriki kibao kutoka ndani na nje ya nchi.

Petro ambaye ni mwanariadha wazamani wa kimataifa wa Tanzania, anasema kuwa wakimbiaji nyota karibu wote nchini wamethibitisha kushiriki mbio hizo, ambazo huanzia katika lango kuu la kuingilia na kutokea katika Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro.

Anasema kuwa hivi karibuni watamtangaza mgeni rasmi wa mbio hizo, ambazo mbali na kupiga vita ujangili wa wanyama pori, pia zinatumika kuinua vipaji vya wanariadha nchini wa rika tofauti tofauti.

KUONGEZWA ZAWADI
Anasema kuwa ili kuongeza msisimko na ushindano wa mbio hizo wameandaa zawadi, ambapo sasa washindi wengi watazawadi tofauti na huko nyuma, ambapo watu wachache wa kwanza ndio walizawadiwa.

Alisema kuwa baada ya kutafakari sasa washindi wengi wa mbio za kilometa 21 watapata zawadi ili kuongeza ushindani na kuvuta washiriki wengi.

Mshindi wa kwanza ataondoka na kitita cha Sh milioni 1 huku wa pili Sh 500,000 wakati yule watatu atapata Sh 250,000, ambapo zawadi zitatolewa hadi kwa mwanariadha wa 10 bora.

Huku kwa watoto wadogo, ambao watashiriki mbio za kilometa 2.5 zawadi zitatolewa hadi tano bora wakati huko nyuma walikuwa wakipata zawadi washindi watatu tu wa kwanza.

Kingine kikubwa katika mbio nyingi washindi wa kilometa tano hawapati zawadi, lakini Ngorongoro Marathon hutoa kifuta jasho kwa washindi wa mbio hizo, ambazo huitwa za kujifurahisha.

ADA ZA USHIRIKI
Kwa washiriki wakilometa 21 kila mshiriki atatakiwa kulipia Sh 10,000 kwa Raia wa Watanzania wakati raia wakigeni akila mmoja atalipa mkiasi cha dola za Marekani 50 wakati watoto watakimbia bure.

Wale watakaoshiriki mbio za kilometa tano watalipia kiasi cha Sh 10,000 kwa watanzania wakati wagemi watalipa dola 10 na timu, yaani kampuni kama itapeleka wafanyakazi wake kushiriki, basi itatakiwa kulipia dola za Marekani 500.

MBIO ZA MWAKA HUU
Wanyama kama tembo, kifaru wamekuwa wakiuawa na majangili kwa ajili ya meno yao wakati twiga na pundamilia wanauawa kwa ajili ya nyama zao huku simba na chui wanapata majanga kutokana na ngozi zao, hivyo mbio za mwaka huu zinaendeleza kampeni ya kupiga vita ujangili huo.

Waandaaji wameamua kupambana na ujangili huo ili kuwaepusha wanayama hao na janga la kuawa kwani wakimalizika, taifa litakosa fedha za kigeni kupitia katika utalii wa kuangalia wanyama.

Mbio hizo zilianza tangu mwaka 2008 na lengo likiwa ni kupiga vita tatizo la taifa na dunia la kuuawa ovyo wanyama kwa ajili ya pembe na ngozi zao.

Huko nyuma lengo lilikuwa kupiga vita malaria katika eneo la Karatu na vitongioji vyakle pamoja na gonjwa hatari la ukimwi, lakini baada ya kupungua kwa tatizo hilo, 

Wamekua wakipiga vita ujangili, ambao umekithiri katika mbuga zetu hapa nchini.
Mbio hizo mwaka huu zinatimiza miaka 11 tangu kuanzishwa kwake na zimekuwa zikiandalia kwa umakini mkubwa chini ya Petro pamoja na Mkurugenzi wa Ufundi, Filbert Bayi, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC).

No comments:

Post a Comment