Monday 9 April 2018

Mlandege Yapokea Kichapo Zanzibar


Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
LIGI Daraja la Kwanza Kanda ya Unguja iliendelea juzi kwa kupigwa michezo mitatu na miwili ikishindwa kuchezwa baada ya viwanja vilivyopangwa kuchezewa kujaa maji.

Michezo iliyochezwa ni ile ya Mlandege iliyocheza na White Bird katika Uwanja wa Amani , Kimbunga na Strongfire ambao ulichezwa Uwanja wa Tazari na Polisi Bridge ilicheza na Idumu  Mchangani.

Mlandege katika mchezo wake alifungwa mabao 2-1 wakati Kimbunga iliifunga Strong Fire mabao 4-2, huku Polisi Bridge in Idumu wakatoka sare ya kutokufungana.

Katika mchezo huo, White Bird iliyokuwa ugenini  ikajipatia ushindi huo kupitia kwa wafungaji wake Mussa Khamis na Januari Yona.

Mlandege ambayo licha ya kufungwa bado inaendelea kuongoza ikiwa na pointi 60, bao lake yalifungwa na Omar Makame.

Michezo ambayo haikuchezwa ni ile iliyopangwa kuchezwa katika Uwanja wa Mwanakombo, ambako kulikuwa na mchezo kati ya Mahonda Kids na Ngome na Miembeni  na Mundu kwenye Uwanja wa Chukwani.

No comments:

Post a Comment