Wednesday 11 April 2018

Wachezaji wa Cameroon Wajilipua Madola Australia


GOLD COAST, Australia
WACHEZAJI nane wa timu ya Cameroon inayoshiriki Michezo ya 21 ya Jumuya ya Madola inayoendelea hapa, wametoweka katika makazi yao, viongozi wa timu wamesema.

Msemaji wa timu hiyo Simon Molombe viongozi walibaini kutokuwepo kwa wachezaji hao na wameripoti tukio hilo kwa polisi ya Australia.

Wachezaji hao watatu ni wa kunyanyua vitu vizito na mabondia watano, ambao kwa mara ya mwisho walionekana Jumatatu na Jumanne.

Cameroon imesema kuwa kundi la wachezaji hao lilikuwa na viza halali ya Australia hadi Mei 15 mwaka huu.

Viongozi wa timu hiyo waliwataja wachezaji hao waliopotea kuwa ni wanyanyua vitu vizito Olivier Matam Matam, Arcangeline Fouodji Sonkbou na Petit Minkoumba, wakati mabondia ni Christian Ndzie Tsoye, Simplice Fotsala, Arsene Fokou, Ulrich Yombo na Christelle Ndiang.
"Mamlaka imesikitishwa sana na kitendo cha wachezaji hao waliotoweka, wengine wakiwa hata bado hawajaanza kushindana, “alisema Molombe.

"Tunatarajia watarudi kijijini na kurudi nyumbani na wenzao.”
Serikali ya Australia imewaonya wachezaji dhidi ya kukaa ndhini humo baada ya kumalizika kwa viza zao.

Shirikisho la Jumuiya ya Madola limesema kuwa watafuatilia hali hiyo lakini walisema kuwa wachezaji wana “haki ya kusafiri huru” kwa kuwa wana viza zao.

Mwaka 2012, wachezaji saba wa Cameroon walitoweka wakati wakiwa jijini London walipokwenda na timu yao kushiriki Michezo ya Olimpiki.

No comments:

Post a Comment