Wednesday 11 April 2018

AS Roma Yaifungisha Virago Barcelona Ulaya


ROME, Italia
HAKUNA aliyetarajia Barcelona inaweza kutolewa na AS Roma katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya baada ya vinara hao wa La Liga kuwa mbele kwa mabao 4-1 baada ya kushinda katika mchezo wa kwanza.

Hata hivyo, Barcelona imefungishwa virago baada ya kupokea kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa Roma katika mchezo ambao wenyeji ndio walikuwa wenyeji. Roma imesonga mbele kwa faida ya bao la ugenini.

Kiungo wa Barca Andres Iniesta alikuwa hataki kukubali kama timu yake imepokea kichapo hicho, ambacho kimeitoa katika mbio za kuwania taji la Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Wakati Iniesta akishindwa kuamini kilichotokea kwa timu yake, mchezaji mwenzake wa timu hiyo, Sergio Busquets amekiita kipigo hicho kuwa ni kibaya zaidi katika historia yake ya soka.

Awali, safari ya Barca kucheza nusu fainali ilionekana kuiva wakati timu hiyo ilipouanza mchezo huku ikiwa na faida ya mabao 4-1, lakini walionesha kiwango kibovu kabisa msimu huu, katika mchezo huo uliofanyika kwenye Uwanja wa Olimpiki.

Baracelona imetupwa nje kwa mabao ya AS Roma yaliyofungwa na Edin Dzeko, Daniele De Rossi kwa penalti na na lile la kichwa lililopachikwa na Kostas Manolas header.

"Inauma kwasababu hakuna mtu aliyetarajia kichapo hiki baada ya kuwa na faida ya mabao manne tuliyopata kutoka katika mhezo wa kwanza, lakini hilo ndilo linakufanya kutambua maana ya michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya, “alisema.

Kufungwa huko kwa Barcelona kumeshuhudia timu hiyo ikitolewa katika hatua ya robo fainali ya mashindano hayo kwa mara ya tatu mfululizo na kukatisha ndoto zao za kushinda mataji matatu msimu mmoja.

"Ni ngumu kukubali kutolewa huku kwasababu tulikuwa na matumaini kibao msimu huu na kwa mara nyingine tena (Ligi ya Mabingwa) imetuacha solemba, “aliongeza kiungo huyo.

"Inasikitisha sana baada ya kuwa na msimu mzuri. Sasa tumepata pigo.”

Nahodha huyo wa Barca alibainisha kuwa huenda mwishoni mwa msimu huu akaondoka katika klabuhiyo aliyoitumikia kwa muda mrefu na kwenda China kucheza soka, ambako ataufurahisha moyo wake.

"Ni usiku mzito, huzuni na tunatakiwa kuomba radhi kwa mashabiki wetu kwa jisi tulivyoangua, “alisema.

"Hli ni pigo kubwa ambalo nimewahi kulipa katika kipindi chote nilichokuwa Barcelona kwasababu jinsi kilivyotokea.”

Barcelona, ambao ni mabingwa mara tano pia walifungwa 3-0 katika hatua kama hiyo ya robo fainali msimu uliopita walipocheza dhidi ya Juventus.

"Nitakuwa muongo kama nitasema kuwa eti tutatumia kipigo hicho kama somo kwasababu mwaka jana tulitolea kwa njia kama hii hii, “aliongeza Busquets.

"Matokeo yetu Ulaya katika miaka miwili iliyopita yamekuwa mabaya sana, kama tunataka kushinda Ligi ya Mabingwa wa Ulaya, basi tunatakiwa kubadilika kabisa.”

No comments:

Post a Comment