Friday 6 April 2018

Wababe wa Yanga Wakiona Chamtema Kuni


Na Mwandishi Wetu
TIMU ya Singida United ambao Jumapili iliyopita iliifunga Yanga kwa penalti 4-2 na kuitoa katika mashindano ya Kombe la Shirikisho la Azam, jana walikiona cha moto baada ya kufungwa 3-0 na Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Kwa ushindi huo, Mtibwa Sugar imefikisha pointi 30 na kuendelea kuwa katika nafasi ya sita huku wanyonge Singida wawakibajki katika nafasi ya tano na pointi zao  35.

Kelvin Sabato ndiye aliyekuwa wa kwanza kuifungia bao Mtibwa katika katika dakika ya 22 katika mchezo huo uliofanyika kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida.

Bao la pili la Mtibwa Sugar lilifungwa na  Kihimbwa katika dakika ya 53 wakati la tatu, liliwekwa kimiani na Hassan Dilunga kwa penalti katika dakika ya 71 baada ya mchezaji mmoja wa Mtibwa kuchezewa vibaya katika eneo la hatari.

No comments:

Post a Comment