Wednesday 11 April 2018

Klopp Awasifia Liverpool kwa Kuifunga Tena City


MANCHESTER, Liverpool
KOCHA wa Liverpool Jurgen Klopp ameimwagia sifa timu yake baada ya kupenya na kutinga nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya baada ya kuifunga tena Manchester City kwa mabao 2-1 katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Etuhad.

Kwa matokeo hayo, Liverpool imesonga mbele kwa ushindi wa jumlaya mabao 5-1, kufuatia ushindi wa timu hiyo katika mchezo wao wa kwanza wa mabao 3-0.

"Tumefunga mabao matano dhidi ya Man City na tumeruhusu kufungwa bao moja tu. Kwa kweli idadi kama hii ya mabao haiwezekani kirahisi, “alisema kocha huyo Mjerumani.

"Vijana walipata soluhisho katika kipindi cha pili. Tayari katika kipindi cha kwanza ulikuwa na nafasi mbili au tatu hivi, hivyo ilikuwa rahisi kwangu na vijana kuona muendelezo wa mchezo. Tukafanikiwa kupata mabao.”

Bao la mapema la Gabriel Jesus liliwapa matumaini Manchester City kama wanaweza kupindua matokeo ya awali na kuibuka na ushindi mnono, ambao ungewapeleka katika nusu fainali, lakini hilo halikufanikiwa.

Badala yake, bao la Mohamed Salah katika dakika ya 39 liliiweka Liverpool kukontroo mpira kabla Roberto Firmino hajakamilisha na kuiwezesha Liverpool kutinga kwa maraya kwanza nusu fainali katika kipindi cha muongo mmoja.

Liverpool kwa mara ya mwisho ilicheza fainali ya Ligi ya Mabigwa wa Ulaya katika msimu wa mwaka 2007-08 na ni matumainiyake sasa yameongezeka baada ya kutolewa kwaBarcelona.

Vigogo hao wa Hispania walitolewa baada ya kufungwa 3-0 na AS Roma, huku Roma ambayo ni timu ya zamani ya Salah imesonga mbele kwa bao la ugenini kufuatia sare ya jumla ya mabao 4-4.

Klopp alisema kutolewa kwa Barcelona: "Kumeinua ari kwa timu zilizobaki.
"Sio kuidharau AS Roma. Walimpoteza Salah na sasa wako katika nusu fainali. Hicho ni kitu kingine.

"Mashindano haya yametenda haki na nilitarajia fainali ya kawaida kabisa kati ya Manchester City dhidi ya Barcelona, na sasa wote wametolewa.

"Lakini sasa kutakuwa na timu mbili zenye nguvu pamoja na kuongeza AS Roma na sisi. Tutaona nini kitatokea lakini na hicho sio kitu cha mimi kufikiria.”

Kocha wa Man City, Pep Guardiola aliwataka wachezaji wake kurejea kiakili katika hali ya kawaida baada ya kuwa na wiki mbaya ya msimu baadaya kutolewa kwa mara ya tatu mfululizo.

Man City ilipata pigo jingine mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kushuindwa kutangaza ubingwa wa Ligi Kuu baada ya kufungwa na majirani zao wa Manchester United.

City ina pointi 13 kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England na kilichobaki ni muda tu kabla timu hiyo haijavikwa taji la England.

Guardiola anataka wachezaji wake kufanya kweli katika mchezo ujao wa Ligi Kuu dhidi ya Tottenham utakaofanyika Wembley Jumamosi ili kutangaza ubingwa endapo watashinda.

"Sasa tunatakiwa kwenda Tottenham tukiwa tumebadilika kifikra, “alisema kocha huyo Mhispania.

"Kipindi cha kwanza tulifanya kila kitu, lakini cha pili tulichemsha.”
Guardiola alisema City waliathirika pia na maamuzi mabovu walipocheza dhidi ya Liverpool.

Leroy Sane alifunga na lingefanya matokeo kuwa 2-0 kama sio mwamuzi kulikataa bao hilo, ambapo Guardiola alililalamikia hadi kutolewa uwanjani.

No comments:

Post a Comment