Monday 16 April 2018

PSG Yatwaa Ubingwa Kiaina Yaichapa Monaco 7-1


PARIS, Ufaransa
KLABU ya Paris St-Germain imetwaa taji la Ligi Kuu ya Ufaransa ya Ligue 1 kiaina, baada ya kuwachapa mabingwa watetezi Monaco kwa mabao 7-1 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Parc des Princes.

PSG inayomilikiwa na raia wa Qatar, imetwaa ubingwa huo baada ya kuongoza kwa pointi 17 dhidi ya Monaco iliyopo katika nafasi ya pili.

Giovani lo Celso na Angel di Maria wote walifunga mabao mawili kila mmoja wakati Edinson Cavani na Julian Draxler nao pia walifunga.

Radamel Falcao alikamilisha ushindi wa PSG wakati Rony Lopes ndiye aliyefunga bao la kufutia machozi kwa Monaco katika mchezo huo uliokuwa wa upande mmoja, ukitawaliwa na washindi.

Monaco ilitwaa taji lake la mara ya kwanza miaka 17 iliyopita katika msimu wa mwaka 2016-17.

Falcao anabaki na Monaco lakini Mbappe – ambaye alijiunga na PSG kwa ada ya pauni milioni 166, awali kwa mkopo, na wachezaji wengine muhimu kama beki Benjamin Mendy aliyeondoka katika klabu hiyo wakati wa majira yaliyopita ya kiangazi.

PSG iliifunga Monaco 3-0 katika fainali ya Kombe la Ligi la Ufaransa mwishoni mwa mwezi uliopita na kiwango chao kimeonekana kuongezeka.

Beki Mbrail Dani Alves alitoa krosi kwa Muargentina Lo Celso katika dakika ya 14 na kuifungia timu yake.

Mchezaji wa kimataifa wa Uruguay, Cavani aliongeza la pili kwa shuti kali la kichwa akiunganisha krosi ya winga Mjerumani Draxler kabla Di Maria hajafunga.

PSG ilimteua kocha wazamani wa Sevilla Unai Emery kama kocha wao mpya kwa miaka miwili kuanzia Juni 2016 na msimu mmoja baadae alitarajiwa tofauti na ilivyofikiriwa ametwaa taji.

Hatahivyo, PSG imesikitishwa na kutolewa katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya kutoka kwa Real Madrid na kuacha swali kuhusu hatma yake.

Inatarajia kuwa Emery ataondoka klabuni hapo mwishoni mwa msimu, huku kocha wazamani wa Borussia Dortmund Thomas Tuchel ndiye anayefikiriwa kubeba mikoba hiyo.

No comments:

Post a Comment