Wednesday 11 April 2018

Ndege Yaanguka Algeria Leo, Yaua Watu 257


ALGIERS, Algeria
WATU 257 wamekufa baada ya ndege ya jeshi kuanguka Kaskazini ya Algeria, wizara ya ulinzi inasema.

Tukio hilo limetokea muda mfupi baada ya ndege kuondoka kutoka katika kiwanja cha ndege cha jeshi cha Boufarik kilichopo jirani na mji mkuu wa Algiers asubuhi.

Wengi waliokufa ni askari na familia zao, kwa mujibu wa wizara ya ulinzi. Wafanyakazi 10 wa ndege hiyo nao waliuawa katika ajali hiyo.

Hatahivyo, bado haijawekwa wazi kilichosababisha ajali hiyo.
Kiongozi wa jeshi ameamuru kufanyika kwa uchukuzi ili kujua chanzo cha ajali hiyo, na aliahidi kutembelea eneo la tukio.

Ndege nyigine iliyoua watu wengi tangu Julai mwaka 2014,ilitokwa wakati watu  298 waliokuwa ndani ya ndege ya Malaysia Airlines namba MH17 walipokufa wakati ilipotunguliwa mashariki ya Ukraine.

Hiyo ilikuwa ajali ya pili kuuawa watu wengi katika ajali ya ndege tangu mwaka 2003.

Mamlaka zinafanyia kazi kutambua mahiti  ya waliokufa katika ajali hiyo. Picha za video kutoka eneo la tukio linaonesha moshi ukitoka katika mabaki ya ndege hiyo.
Ndege hiyo aina ya Ilyushin Il-76, ilikuwa ikisafiri kutoka Bechar kusini-magharibi ya nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment