Sunday 28 January 2018

Kocha wa Simba Aipeleka Sudan Nusu Fainali Chan

CASSABLANCA, Morocco
SUDAN na wenyeji Morocco wametinga nusu fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan 2018) baada ya kushinda mechi zao.

Sudan ambayo inafundishwa na kocha wazamani wa Simba, Zdravko Logarusic (pichani), imetinga nusu fainali baada ya kuifunga Zambia bao 1-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Marrakech hapa.

KUJIUNGA NA SIMBA
Baada ya kuondoka Simba, kocha huyo alipewa ofa nono na klabu ya Simba Sports Club ili kuifundisha timu yao.

Alipotua Simba klabu hiyo ilimpatia mshahara mnono pamoja na nyumba eneo la ufukweni mwa Bahari ya Hindi.

Hatahivyo, kwa bahati mbaya, kocha huyo alikuwa hajui Kiswahili na kumfanya kushindwa kuwasiliana vizuri na vyombo vya habari vya Tanzania, ambapo baada ya nusu mwaka alivunjiwa mkataba.

Logarusic alikuwa akiidai Simba kiasi cha Sh milioni 3.6 kutokana na klabu hiyo kuvunja mkataba huku klabu ikidai kuwa eti ni madai ya uongo.

Bao lililofungwa katika kipindi cha kwanza na Malik Saifeldin na kudhihirisha nia yao ya kucheza hatua ya nne bora.

Sudan watacheza nusu fainali ya pili itakayopigwa Jumatano, ama na Nigeria au Angola.

Zambia ambao wanajulikana kama Chipolopolo walifugwa bao hilo pekee katika dakika ya 32 na kufanya Sudan kuwa katika nafasi nzuri ya kusonga mbele.

Hatahivyo, Zambia ilizinduka muda mfupi baadae, baada ya timu hiyo kufanya shambulizi la nguvu baada ya kocha Wedson Nyirenda kumbadili Mwengani na kuingia kiungo Jackson Chirwa, na kuiongezea nguvu timu hiyo ya Kusini mwa Afrika.

Katika mchezo wa awali, wenyeji Morocco walikuwa wa kwanza kukata tiketi ya kucheza nusu fainali baada ya kuifunga Namibia 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Stade Mohamed V jijini hapa juzi jioni.


Mabao yaliyofungwa katika kila kipindi cha mchezo kutoka kwa Ayoub El Kaabi na Salaheddine Saidi kulishuhudia Simba wa Atlas wakistahili ushndi dhidi ya Namibia.

No comments:

Post a Comment