Saturday 20 January 2018

Chelsea Yatoa Kipigo Kizito EPL cha Mabao 4-0

Beki wa Brighton, Markus Suttner (kushoto) akiwania mpira na kiungo wa Chelsea, Eden Hazard wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya England kwenye Uwanja wa  American Express Community huko Brighton, kusini ya England jana. Chelsea ilishinda mabao 4-0. (Picha na AFP).
LONDON, England
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Chelsea jana walitoa kichapo kikali kwa Brighton & Hove Albion baada ya kuitandika mabao 4-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Community.

Kwa ushindi huo, Chelsea imefikisha pointi 50 na kuwa katika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo inayoshirikisha timu 20.

Liverpool endapo itashindamchezo wake wa leo dhidi ya Swansea City kwenye Uwanja wa Liberty, nayo itafikisha pointi 50, lakini zitakuwa zikishindana kwa mabao ya kufunga na kufungwa.


Mabao ya Chelsea jana yalifungwa na Eden Hazard mawili huku mengine yakiwekwa kimiani na Willian na Moses.

No comments:

Post a Comment