Friday 5 January 2018

Mohamed Salah Mwanasoka Bora wa Afrika 2017

Rais wa Shirikisho la Soka la Afrika (Caf), Ahmad Ahmad (kulia) akimkabidhi tuzo mwanasoka bora wa mwaka wa Afrika, mshambuliaji wa Misri na Liverpool, Mohamed Salah wakati wakukabidhi tuzo hiyo mjini Accra, Ghana jana.
ACCRA, Ghana
HAYAWI hayawi yamekuwa; hatimaye mshambuliaji wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri, Mohamed Salah ametangazwa kuwa mchezaji bora wa Afrika katika tuzo za Shirikisho la Soka la Afrika (Caf) zilizofanyika mjini hapa usiku wa jana.

Mchezaji amepewa tuzo hiyo kwa mafanikio aliyoyapata mwaka 2017.

Salah amekuwa na mwaka mzuri sana ndani ya 2017 akizisaidia timu yake ya taifa ya Misri kufuzu Kombe la Dunia, huku akiwa wa pili kwa mabao katika Ligi Kuu ya England (EPL), ambapo mwaka 2017 alifunga jumla ya mabao 39 na kusaidia mara 18.

Timu ya taifa ya Misri ambao ndio mabingwa wa soka barani Afrika walitangazwa kuwa timu bora Afrika huku tuzo ya mshambuliaji chipukizi ikienda kwa kinda raia wa Ivory,  Coast Patson Daka.

Wakati Misri wakipata tuzo ya timu bora, kocha wao Hector Cupper alitwaa tuzo ya kocha bora, huku tuzo ya mwanasoka bora Afrika kwa upande wa wanawake ikienda kwa Mnigeria Asisat Oshoala.



No comments:

Post a Comment