Friday 19 January 2018

Tigo yatangaza Zawadi Nono za Kili Marathon 2018

Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya simu za Mkononi ya Tigo Kanda ya Kaskazini, Henry Kinabo akizungumza wakati wa uzinduzi wa Msimu wa 16 wa Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro Marathon 2018,Uzinduzi uliofanyika katika Hoteli ya Kibo Palace Homes mjini Moshi juzi, Mashindano ambayo Kampuni ya Tigo inadhamini Mbio za Nusu Marathon,Km 21. Pichani (mwenye kofia) Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira na wadau mbalimbali. (Na Mpigapicha Wetu).
Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Simu za mkononi ya Tigo imesema kuwa itadhamini tena mbio za nusu marathon za Kilimanjaro zitakazofanyika Machi 4 mjini Moshi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mbio hizo juzi, Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya simu za Mkononi ya Tigo Kanda ya Kaskazini, Henry Kinabo alisema wanadhamini tena mbio hizo kwa mwaka wanne mfululizo.

Kinabo alisema wanaunga mkono mbio hizo, ambazo zinasaidia kuibua na kuviendeleza vipaji vya vijana na kuhakikisha Watanzania wanaishi katika maisha ya kiafya kwa kushiriki katika mchezo huo wa riadha.

Alitaja zawadi, ambazo zitatolewa kwa washindi wa kwanza kwa upande wa wanawake na wanaume, kila mmoja ataondoka na kitita cha sh milioni 2.

Huku washindi wa pili kila mmoja tazawadiwa sh milioni 1 huku mshindi watatu ataondoka n ash 650,000, wanne sh 500,000, mshindi wa sita sh 325,000 wakati wasabi atapewa sh 250,000.


Alisema kuwa mshindi wanane ataondoka na kiasi cha sh 150,000, huku mshindi wa tisa atapewa sh 125,000 na wa 10 atabeba sh 100,000.

No comments:

Post a Comment