Sunday 28 January 2018

Caroline Wozniacki Bingwa Australian Open 2018

MELBOURNE, Australia
CAROLINE Wozniacki amesema kuwa amefurahishwa kwa kuwa sasa hataulizwa tena kuhusu kutopata mataji ya mashindano makubwa baada ya juzi kushinda Australian Open.

Mdenish huyo mwenye umri wa miaka 27, alimchakaza Simona Halep kwa 7-6 (7-2) 3-6 6-4 katika mchezo wa fainali uliofanyika hapa na hatimaye kupata taji lake kubwa la kwanza katika majaribio 43.

Licha ya kumaliza mwaka akiwa katika nafasi ya kwanza duniani mwaka 2010 na 2011, mchezaji huyo alikosa mataji manne makubwa.

"Hata ni mambo mazuri sana kwangu, “alisema Wozniacki.

"Kuanzia sasa kamwe sitaulizwa maswali kama hayo tena. Nasubiri maswali, ‘Lini utakwenda kushinda tajila pili?'

Leo Jumatatu, Wozniacki atarejea kileleni katika viwango vya ubora tangu alipokuwa namba moja kwa mara ya mwisho.

"Ni wazi hilo ni jambo maalum,”aliongeza.

"Nafikiri kuwa bingwa mpya wa mashindano makubwa na bingwa namba moja kwa ubora dunani ni jambo zuri. Nimefurahishwa sana na hilo. Kwa kweli ndoto imetimia.”

Wozniacki ni Mdenish wa kwanza kushinda taji kubwa la mchezaji mmoja mmoja, na kuwa nyuma ya Jana Novotna (45), Marion Bartoli (47) na Flavia Pennetta (49) ambao walishiriki mara nyingi kabla ya kutwaa mataji makubwa.

Pia kwa ushindi huo ameondoka na kitita cha pauni milioni 2.3.


Wozniacki alipongezwa katika mitandao ya kijamii na Serena Williams, ambaye alishindwa kutetea taji lake la Australian Open miezi minne kabla ya kujifugua mtoto wake wa kwanza.

No comments:

Post a Comment