Sunday 21 January 2018

George Weah Apiga Bao Akijiandaa Kuapishwa Kuwa Rais wa Liberia

Rais Mteule wa Liberia, George Weah (kushoto) akimiliki mpira wakati wa mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Jeshi uliofanyika jana. Weah anatarajia kuapishwa kesho mjini Monrovia kwa rais rasmi wa nchi hio.
MONROVIA, Liberia
GEORGE Weah alifunga bao la kipindi cha kwanza na kuiongoza timu ya Weah All Stars kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya timu ya Jeshi la Liberia katika mchezo wa kuelekea kuapishwa kwa rais mpya wa nchi hiyo mjini hapa.

Weah anaapishwa rasmi kesho kuwa rais mpya wa Liberia baada ya kushinda uchaguzi hivi karibuni.

Mchezo huo ulikuwa sehemu ya program ya hafla ya kuapishwa kwa Weah mwenye umri wa miaka 51, ambaye ni mchezaji soka nyota wazamani, ambaye Desemba alichaguliwa kuwa rais wan chi hiyo.
"Asili ya mchezo ni kushinda, “alisema Weah alipozungumza na BBC Sport baada ya mchezo huo wa maonesho.

Weah alikuwa amevaa jezi namba 14 ya asili, akiwakubusha watazamaji ugwiji wake wa soka wakati akivaa jezi namba hiyo ya timu ya taifa ya Liberia, ambako aliifungia Lone Stars mabao ya kukumbukwa.

"Hii ni namba yangu, nambayo nilipewa na taifa, hivyo nimeivaa, “alisema.

Mchezo huo ulichezwa chini ya ulinzi mkali tena wakati wa jua kali, ambapo mamia ya watu walifurika kwenye uwanja huo uliopo katika kambi ya jeshi kumshuhudia mchezaji bora wa dunia wa mwaka.
Huku bandi ya jeshi ikitumbuiza pembeni ya uwanja, Weah aliamsha hisia za mashabiki pale alipowapita wachezaji wa timu pinzani.

Bao lake lilipatikana katikakipindi cha kwanza kwa mkwaju wa adhabu baada ya shuti lake kubadili mwelekeo na kujaa kushoto ya lango.

"Tumekuja kushinda, hii sio ndoto, “alisema, akitembea pembeni ya mkuu wa majeshi, Meja Jeneral Daniel Ziankahn.

"Wachezaji wa jeshi wanaweza kukimbia, wana nguvu zaidi yetu, lakini tulipiga mpira vizuri na tulijipanga vizuri pia.

"Tulitumia udhaifu wao, kwa upande wa ufundi na kwa kweli kifundi tulikuwa wazuri zaidi yao, “aliongeza Weah.
Timu ya Weah All Star iliundwa na wachezaji wenzake wazamani wa timu ya taifa, ambao walimuunga mkono katika mbio za kusaka urais.

Mmoja wao alikuwa mshambuliaji wazamani wa Arsenal Christopher Wreh, ambaye alicheza pamoja na George Weah katika klabu yake ya kwanza Ulaya, AS Monaco.

"Ni siku maalum kwa sababu baada ya leo itakuwa ngumu sana kukutana naye (Weah), “alisema Wreh alipozungumz na BBC Sport.


"Leo najivunia kuwa wote kati yetu tumemzunguka akielekea kuwa rais wa Liberia, “alisema.

No comments:

Post a Comment