Sunday 28 January 2018

Bayern Munich Yatoka Nyuma na Kushinda 5-2

BAYERN, Ujerumani
BAYERN Munich imeibuka na ushindi wa mabao 5-2  licha ya kuwa nyuma kwa mabao mawili baada ya dakika 12 na kuifunga Hoffenheim na kuongeza uongozi wake katika Bundesliga na kufika pointi 16 zaidi.

Vinara hao walijikuta wakiwa nyuma kwa mabao yaliyofungwa na Mark Uth na winga wazamani wa Arsenal Serge Gnabry, ambaye naichezea kwa mkopo Hoffenheim kutoka Bayern.

Lakini mabao kutoka kwa Robert Lewandowksi na Jerome Boateng yaliwawezesha wenyeji kuwa sre zikiwazimebaki dakika 25 kabla ya mchezo kumalizika.

Juhudi za Kingsley Coman na Arturo Vidal ziliiweka Bayern Munich kuwa mbele baada ya mapumziko.


Sandro Wagner aliongeza bao la tano kwa vinara hao wa ligi.

No comments:

Post a Comment