Friday 26 January 2018

Kambi ya Riadha Kuanza Jumatatu Kilimanjaro

Na Mwandishi Wetu
KAMBI ya timu ya taifa ya riadha kwa ajili ya mashindano mbalimbali ya kimataifa, inatarajia kuanza Jumatatu West Kilimanjaro wilayani Siha.

Kambi hiyo ambayo awali ilitakiwa kuanza Januari 15, ilishindwa kuanza kutokana na kutokamilika kwa baadhi ya taratibu.

Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania (RT), Wilhelm Gidabuday alisema jana kuwa sasa kambi hiyo itaanza rasmi Jumatatu, Januari 29, ambapo wanariadha 15 na makocha wanne watakuwepo.

Alisema kuwa wanariadha hao ni wale watakaoshiriki mashindano tofauti ya kimataifa, ikiwemo mashindao ya dunia ya nusu marathon, Jumuiya ya Madola pamoja London Marathon

Alisema kuwa mashindano ya dunia ya nusu marathon yatafanyika Valencia, Hispania Machi 24 kabla ya kufanyika Michezo ya Juuiya ya Madola kuanzia Aprili 4 hadi 15.

Alisema kuwa mashindano watakaoshiriki wanaridha hao ni yale ya London Marathon, ambayo mbali na Alphonce Simbu pia RT itapeleka wanariadha wengine kwa ajili ya mbio hizo.


Aidha, Gidabuday amesma kuwa makocha Zacharie Barie na Lwiza John ndio wataongoza na timu ya riadha katika Michezo ya Jumuiya ya Madola.

No comments:

Post a Comment