Sunday 21 January 2018

Wababe wa Yanga Wachapwa na Vibonde Stand

Na Mwandishi Wetu, Mwanza
WACHOVU wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Stand United ya Shinyanga (pichani)  imewazima wababe wa Yanga, Mbao FC baada ya kuwafunga bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu uliofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini hapa.

Mbao FC wiki iliyopita ilitoa kipigo kwa mabingwa watetezi Yanga baada ya kushinda mabao 2-0 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, lakini wamejikuta wakishindwa kuibuka na pointi tatu au moja dhidi ya vibonde Stand United, ambao kabla ya mchezo huo walikuwa wakikalia mkia na pointi zao 10.

Ushindi huo umeibena Stand United hadi kufikia nafasi ya 11 kati ya timu 16 zinazoshiriki ligi hiyo.
Ushindi huo unaifanya Stand United ifikishe pointi 13 baada ya kucheza mechi 14 na kusogea juu hadi nafasi ya 11 kutoka mkiani kwenye ligi ya timu 16.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Jacob Adongo aliyesaidiwa na Hellen Mduma na Martin Mwalyaje, Stand United walipata bao lao dakika ya 40 likifungwa na Vitalis Mayanga kwa penalti baada ya kipa wa Mbao, Ivan Rugumandiye kumkamata miguu Landry Ndikumana baada ya wote kuanguka wakati wanawania mpira ndani ya boksi.


Katika mchezo mwingine leo, Mtibwa Sugar imelazimishwa suluhu na Njombe Mji FC kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro. 

No comments:

Post a Comment