Saturday 20 January 2018

Shimiwi Kuandaa Bonanza Kubwa Dodoma

Uongozi mpya wa Shirikisho la Michezo la Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) mara baada ya kutangazwa na msimamizi wa uchaguzi uliofanyika hivi karibuni kwenye hoteli ya Mount Uluguru mkoani Morogoro.
Na Mwandishi Wetu
SHIRIKISHO la Michezo la Wizara na Idara za Serikali (Shimiwi) linatarajia kuandaa bonanza kubwa la kwanza la michezo mkoani Dodoma litakalofanyika mwezi ujao.

Katibu Mkuu wa Shimiwi, Moshi Makuka alisema jana kuwa, bonanza hilo la michezo ni kwa ajili ya kulitambulisha shirikisho hilo mkoani humo, hasa ukizingatia ndio Makao Makuu ya nchi na wafanyakazi wengi wa Serikali wako huko sasa.
Makuka alisema kuwa baada ya Dodoma, bonanza hilo litahamia jijini Dar es Salaam, ambako wafanyakazi wa Serikali watashiriki katika michezo mbalimbali.

Alisema kuwa kamati yao ya utendaji ilikutana hivi karibuni, ambapo pamoja na mambo mengine ilijadili pia utekelezaji wa akizo la Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan la kufanya mazoezi kila wiki ya pili ya kila mwezi, ili kuweka fiti afya za wafanyakazi.

Pia walijadili jinsi ya kukiendeleza kiwanja chao cha Bunju B jijini Dar es Salaam, ambapo mbali na kujenga uwanja wa michezo, pia kutakuwa na hosteli na kumbi kwa ajili ya shughuli mbalimbali, ambazo zitawaingizia kipato.

Aidha, kikao hicho kiliunda kamati mbalimbali ikiwemo ya habari na mawasiliano kwa ajili ya kulitangaza shirikisho hilo kwa wadau mbalimbali.

Alisema waandishi wa habari za michezo wa Kituo cha Televisheni cha Taifa (TBC), Jane John na Jessey John  na  Ofisa Uhusiano wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bahati Mollel ni miongoni mwa wanaounda kamati hiyo.
Makuka alisema wanataaluma hao wa habari, ambao pamoja na kuwa ni wachezaji katika timu za wizara zao, wamekuwa pia wakitoa michango mikubwa katika kutangaza na kuandika habari za Shimiwi.

Wengine waundao kama hiyo ni pamoja na Itika Mwankenja (Mwenyekiti), Elias Malima (katibu) na wajumbe ni James Katubuka na David Kitila.
Kamati ya Utendaji inaundwa na Daniel Mwalusamba (Menyekiti), Ally Katembo (Makamu Mwenyekiti), Makuka (Katibu Mkuu), Alex Temba (Katibu Msaidizi), William Mkombozi (Mhazini), Frank Kibona (Mhazini Msaidizi).

Wajumbe ni Appolo Kayungi, Damian Manembe, Seleman Kifyoga, Assumpta Mwilanga na Aloyce Ngonyani, huku wajumbe wa viti maalum ni Mariam Kihange na Mwajuma Kisengo.

Wanaounda Kamati ya Mipango ni Mwalusamba (Mwenyekiti), Mkombozi (Katibu) na wajumbe ni Makuka, Ngonyani, Kihange na John Jambele; huku kamati ya Ufundi inaundwa na Kayungi (Mwenyekiti), Manembe (Katibu) na wajumbe ni Kisengo na Joyce Benjamin; Kamati ya Nidhamu wapo Katembo (Mwenyekiti), Temba (Katibu) na wajumbe ni Marcel Katemba na Mwilanga.

Kamati ya usajili itaongozwa na Temba (Mwenyekiti), Kibona (Katibu) na James Emmanuel (Mjumbe); nayo Sekretarieti ya Uendeshaji inaundwa na Kihange (mwenyekiti), Kifyoga (Katibu), na wajumbe ni  Bahati Magambo, Buya Ndalija, Justo Mwandelile, Ahmed Chitagu, Peter Lihanjala, Gracia Kyelula, Peter Onono, Modesta Kaunda, Amina Kakozi, Ismail Ismail, Sophia Mkama na James Emmanuel.
Nayo Kamati ya Huduma za tiba itaongozwa na Joakim Mwaipaja (Mwenyekiti), Magreth Mtaki (Katibu), na Wajumbe ni Richard Yomba, Haji Masasi, Jafari Chikoko na Gration Kaizirege.

No comments:

Post a Comment