Friday 26 January 2018

Kyle Edmund atolewa Australian Open 2018

MELBOURNE, Australia
MUINGEREZA Kyle Edmund amesema kuwa "amepata uzoefu wa kushindana katika mashindano makubwa ya tenisi baada ya kutolewa katika nusu fainali ya Australian Open.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 alishindwa kusonga mbele baada ya kuchapwa kwa 6-2 7-6 (7-4) 6-2 na mchezaji wa Croatia anayeshikilia nafasi ya sita kwa ubora Marin Cilic mjini hapa.

Hatahivyo, Edmund aligoma kulaumu maumivu ya nyonga, ambayo yalihitaji matibabu, lakini alicheza mashindano hayo na kutinga nusu fainali.
"Hatimaye nimetoka baada ya wiki nzimaya kufanya vizuri katika mashindano haya, “alisema Edmund.

"Aina hii ya mashindano inakupa uzoefu zaidi. Kwa mara nyingine tena unapata jaribio, ni kama mwaka, nahitaji kama hii zaidi,”

Cilic, 29, alitawala mchezo wa nusu fainali baada ya kuokoa pointi kibao hadi mapumziko.

No comments:

Post a Comment