Sunday 28 January 2018

Ronaldo Bado Handsome Licha ya Kuumia Usoni

MADRID, Hispania
MCHEZAJI Cristiano Ronaldo anasema kuwa ‘bado ana sura nzuri’ baada ya sura yake kuachwa imejaa damu baada ya kupigwa usoni wakati wakicheza dhidi ya Deportivo La Coruna wiki iliyopita.

Ronaldo alibainisha juzi kuwa bado anataka kubaki Real Madrid licha ya taarifa kuwa hana furaha Hispania.

Picha ilionesha Mreno huyo akijiangalia sura kupitia simu ya mkononi ya daktari wa klabu hiyo wakati akitoka uwanjani akiwa ameumia Jumapili iliyopita kufuatia kugongwa na kupasuka usoni.

Mchezaji huyo ilibidi kushonwa nyuzi tatu juu ya jicho lake wakati akifanyiwa matibabu ya jeraha hilo.

"Wachezaji walinipiga mimi katika mchezo kwa sababu ilibidi wanisimamishe mimi lakini hiyo haikuwa bahati, “alisema Ronaldo katika mahojiano na mtandao wa China wa Dongqiudi.

"Sasa najisikia vizuri, bado nina furaha, bado nina sura nzuri na ninaona vizuri kama mwanzo na hakuna tatizo.”


Ronaldo yuko katika hali mbaya katika soka la nyumbani tangu alipojiunga na Real Madrid akitokea Manchester United mwaka 2009 wakati aliponuliwa kwa rekodi ya dunia ya paui milioni 80 , akifunga mabao sita tu, ingawa anaongoza kwa ufungaji katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

No comments:

Post a Comment