Friday 26 January 2018

Mourinho bado yupo yupo Man United hadi 2020

LONDON, England
KOCHA wa Manchester United Jose Mourinho ameongeza mkataba utakaomuweka katika klabu hiyo hadi mwaka 2020, ukiwa na nafasi ya kuongeza mwaka mmoja zaidi.
Mkataba wa awali wa kocha huyo mwenye miaka 54 Old Trafford unatakiwa kumalizika mwaka 2019.

Mourinho alisema “amefurahi” kuwa Man United “wananiamini kuwa kocha sahihi kwa ajili ya klabu kubwa….”

"Najihisi mtu mwenye bahati kufanya kazi na kundi la vijana wa ajabu, “aliongeza.
"Mkataba wangu wa awali ulikuwa ni wa miaka mitatu, sasa tumefanya uamuzi wa wazi kwa kila mmoja sio miaka mitatu, ni minne au mitano, nani anajua, zaidi.”

Mourinho, aliteuliwa kuwa kocha wa Man United kuchukua nafasi ya Louis van Gaal Mei mwaka 2016, ambapo alishinda Kombe la EFL na lile la Ligi ya Ulaya katika msimu wake wa kwanza.

Msimu huu Man United wako katika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu ya England, wakiwa nyuma ya Manchester City, huku timu hiyo ikiwa bado iko katika mbio za Ligi ya Mabingwa na Kombe la FA.

"Tumeweka viwango vya juu, tukishinda mataji matatu katika msimu mmoja, lakini hicho ni kiwango nilichotarajia, “alisema kocha huyo Mreno.

Woodward alimpongeza Mourinho kwa kazi yake nzuri na weledi”, wakati akitimiza lengo la klabu kukuza vipaji vya wachezaji chipukizi na wenye viwango”.

Akizungumza mapema juzi katika mkutano na waandishi wa habari, kabla ya kuingia mkataba huo mpya, Mourinho aliipongeza klabuhiyo kwa kumsajili Alexis Sanchez kutoka Arsenal.

Alisema mchezaji huyo wa kimataifa wa Chile amejiunga kutoka klabu ya ajabu na kwenda katika klabu kubwa huku ikishuhudia kiungo wa Armenia Henrikh Mkhitaryan akitua upande mwingine.


Mourinho alisema ni usajili mkubwa kwa kila mtu na kuthibitisha Sanchez atakuwa katika kikosi cha United kilichotarajia kucheza Kombe la FA jana dhidi ya Yeovil.

No comments:

Post a Comment