Friday 26 January 2018

Coutinho aanza kuichezea Barcelona, aingia akitokea benchi wakati wakiifunga Espanyol 2-0

BARCELONA, Hispania
PHILIPPE Coutinho ameanza kuichezea Barcelona wakati timu hiyo ikiifunga Espanyol na kutinga nusu fainali ya Kombe la Hispania usiku wa kuamkia leo.

Mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa ada ya pauni milioni 142 akitokea Liverpool aliingia akitokea benchi zikiwa zimebaki dakika 22 kabla ya mchezo haujamalizika wakati tayari Barcawakiwa mbele kwa mabao 2-0.

Barcelona imesonga mbele kwa ushindi wa jumla ya mabao 2-1 baada ya mchezo wa kwanza kufungwa 1-0.

Coutinho nusura angesaidia kupatikana kwa bao, lakini kipa Pau Lopez aliokoa shuti la Luis Suarez, ambaye awali aliifungia Barca bao la kuongoza dhidi ya wapinzani wao wa jiji.

Lionel Messi alifunga bao safi la pili wakati akitimiza mabao 4,000 kwenye uwanja huo wa Nou Camp.

Sevilla, Valencia na Leganes – ambayo iliitoa Real Madrid Jumatano, ni timu zingine zilizopo katika nne bora.

Kabla ya mchezo huo, beki wa Argentina Javier Mascherano alitoka nje ya uwanja kuaga, baada ya kukamilisha uhamisho wa kwenda kucheza China katika klabu ya Hebei China Fortune.


Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 ambaye aliwahi kuichezea West Ham na Liverpool alitumia miaka nane katika klabu ya Barca, akishinda mataji 18 yakiwemo manne ya La Liga na mawili ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

No comments:

Post a Comment