Monday 8 January 2018

Arsenal Yavuliwa Taji la FA baada ya kipigo cha 4-2

LONDON, England
KOCHA Arsene Wenger amejikuta lawamani baada ya Arsenal kutolewa katika raundi ya tatu ya Kombe la FA na timu ya daraja la kwanza ya Nottingham Forest.

Katika mchezo huo uliofanyika kwenye Uwanja wa City Ground, Arsenal ilijikuta ikipokea kichapo cha mabao 4-2 kutoka kwa timu hiyo ya daraja la kwanza.

Wenyeji Nottingham Forest walipata bao la kwanza wakati Eric Lichaj alipofunga kwa kichwa bao la kuongoza kwa mpira wa karibu wa kichwa.

Hatahivyo, furaha za bao hilo zilidumu kwa dakika tatu tu wakati Per Mertesacker alipofunga bao la kusawazisha katika dakika ya 23 baada ya mpira wa kichwa wa Rob Holding kugonga mwamba.

Lichaj alifunga tena bao la kungoza kwa Forest, ambayo inaongozwa na kocha Gary Brazil, 
ambapo beki huy Mmarekani alifunga ndami ya boksi dakika moja kabla ya mapumziko.

Katia kipindi cha pili, Forest iliongeza kasi wakati Ben Brereton alipompeleka sokoni kipa David Ospina na mpira kujaa wavuni.
Mshambuliaji wa timu ya Daraja la Kwanza ya Nottingham Forest, Ben Brereton (kulia) akishangilia kufungala  penalti likiwa ni la tatu la timu yake walipocheza raundi ya tatu ya Kombe la FA dhidi ya Arsenal jana kwenye Uwanja wa The City Ground. Nottingham ilishinda kwa mabao 4-2.
Danny Welbeck alipunguza kipigo kwa timu ya Wenger ambayo iliundwa na wachezaji wengi wasio wa kikosi cha kwanza baada ya kipa wa Forest Jordan Smith kuhindwa kuzuia shuti hilo.

Hiyo ni mara ya kwanza kwa Arsenal kutolewa katika raundi ya tatu ya Kombe la FA tangu Januari mwaka 1996 waliporudiana na Sheffield United.

Penalti ilizidi kumchefua Wenger, ambaye hivi karibuni alifungiwa na Chama cha Soka (FA) kwa kosa la kuwalalamikia waamuzi.


Katika mchezo huo, Wenger alishuhudia mchezo huo kutokea jukwaani baada ya kufungiwa mechi tatu kukaa katika benchi la timu yake.

No comments:

Post a Comment