Wednesday 23 August 2017

Yanga wasaka kufuta uteja wa kufungwa na Simba

Na Mwandishi Wetu

TIMU za Yanga na Simba leo zinashuka kwenye Uwana wa Taifa kucheza mchezo a Ngao ya Jamii ikiwa ni uzinduzi rasmi wa msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2017/18 utakaoanza wikiendi ijayo.

Hii ni mechi ya tatu kwa kocha wa Yanga, Mzambia George Lwandamina kukutana na watani zake za jadi Simba, huku kocha huyo akifungwa mara mbili na watani hao tangu alioanza kuifundisha Yanga.

Huo utakuwa mchezo wa tatu kwa Mzambia, George Lwandamina tangu achukue nafasi ya Mholanzi, Hans van der Pluijm Desemba mwaka jana na mechi mbili zilizopita zote alipoteza. 

Januari 10, mwaka huu Uwanja wa Amaan, Zanzibar Yanga ilifungwa kwa penalti 4-2 na Simba baada ya sare ya 0-0 katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi.

Februari 26, mwaka huu, Simba ikatoka nyuma na kushinda 2-1 kwa mabao ya Mrundi Laudit Mavugo dakika ya 66 na Shiza Kichuya dakika ya 81, baada ya Simon Msuva kuanza kuifungia Yanga kwa penalti dakika ya tano.

Na mechi zote Lwandamina amefungwa na Simba ikiwa chini ya kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog akisaidiwa na Mganda, Jackson Mayanja ambao wote leo watakuwepo kwenye benchi la Simba,

Katika benchi la Yanga kuna mabadiliko kidogo, kocha msaidizi wa msimu uliopita, Juma Mwambusi hayupo na nafasi yake imechukuliwa na beki na nahodha wa zamani wa timu hiyo, Shadrack Nsajigwa.

Kwenye benchi la Simba, ameondoka kocha wa makipa Mkenya, Iddi Salim na nafasi yake kuchukuliwa na golikipa wa zamani wa timu hiyo, Muharami Mohammed Shilton.

Kiungo Haruna Niyonzima leo ataibukia kwa mahasimu Simba, baada ya miaka sita ya kucheza Yanga tangu alipojiunga nayo mwaka 2012 akitokea APR ya Rwanda. Yanga pia haitakuwa mchezaji wake mahiri na aliyekuwa tegemeo katika safu ya ushambuliaji, Simon Msuva aliyehamia Difaa Hassan El- Jadida ya Ligi Kuu ya Morocco.

Mshambuliaji Ibrahim Hajib naye leo ataibukia kwa watani, Yanga baada ya kuibukia timu ya vijana ya Simba na kupandishwa kikosi cha kwanza cha timu hiyo alikopatia umaarufu. Simba pia haitakuwa na beki wake, Abdi  Banda aliyehamia Baroka FC ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini.

Timu zote zilikuwa kambini upande wa pili wa Muungano wa Tanzania kwa wiki nzima Yanga walikuwa kisiwani Pemba na Simba walikuwa Unguja na kabla ya mchezo wa leo, kila timu imecheza mechi sita za kujipima na kila moja ilipoteza mchezo mmoja.

Simba ilifungwa 1-0 na Orlando Pirates, kabla ya kutoa sare ya 1-1 na Bidvest Wits nchini Afrika Kusini, ikashinda 1-0 na Rayon Sport ya Rwanda, 1-0 na Mtibwa Sugar, 0-0 na Mlandege na kumalizia kwa ushindi wa 5-0 dhidi ya Gulioni FC, wakati Yanga ilishinda 5-0 na Moro Kids, 3-2 na Singida United, ikafungwa 1-0 na Ruvu Shooting, ikashinda 2-0 na Mlandege, 1-0 na Chipukizi na 1-0 na Jamhuri.   

Mara ya mwisho Yanga kuifunga Simba ilikuwa ni Februari 20, mwaka 2016 ushindi wa 2-0 uliotokana na mabao ya mshambuliaji Mzimbabwe Donald Ngoma dakika ya 39 na Amissi Tambwe dakika ya 72, ambao kwa pamoja leo wanatarajiwa kuiongoza tena timu hiyo.

REKODI YA SIMBA NA YANGA NJE YA LIGI KUU:

NANI MTANI JEMBE:

DESEMBA 13, 2014

Simba SC 2-0 Yanga

WAFUNGAJI:

SIMBA SC: Awadh Juma na Elias Maguri

NANI MTANI JEMBE:

DESEMBA 23, 2013

Simba SC 3-1 Yanga

WAFUNGAJI:

SIMBA SC: Amisi Tambwe dk 14 na 44penalti na Awadh Juma dk,

YANGA SC: Emmanuel Okwi dk87 

KLABU BINGWA AFRIKA MASHARIKI NA KATI:

JULAI 10, 2011

Yanga 1-0 Simba, Fainali

MFUNGAJI : Kenneth Asamoah dk 108

JANUARI 1975

Yanga Vs Simba; Fainali, 2-0

WAFUNGAJI: Gibson Sembuli na Sunday Manara

JANUARI 1992

Simba Vs Yanga; Fainali

1-1, Simba ilishinda kwa penalti 5-4

JULAI 27, 2008

Simba Vs Yanga; Mshindi wa Tatu

(Yanga haikutokea uwanjani, Simba ikapewa ushindi wa chee)

KOMBE LA HEDEX:

JUNI 30, 1996

Yanga Vs Simba 2-0

CCM Kirumba, Mwanza

WAFUNGAJI: Bakari Malima na Edibily Lunyamila

KOMBE LA HEDEX:

JULAI 13, 1996

Simba Vs Yanga 1-1, Taifa, Dsm

WAFUNGAJI:

SIMBA: Hussein Amaan Marsha kwa penalti

YANGA: Bakari Juma Malima

KOMBE LA TUSKER:

FEBRUARI 10, 2001

Yanga Vs Simba (fainali) 0-0

(Simba ilishinda kwa penalti 5-4, Uwanja wa Taifa)

MACHI 31, 2002.

Simba Vs Yanga 4-1

WAFUNGAJI:

SIMBA: Mark Sirengo dk. 3 na 76, Madaraka Selemani dk. 32 na Emanuel Gabriel dk. 83.

YANGA: Sekilojo Chambua dk 16.

(Mechi hii ya fainali iliyohudhuriwa na rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, chupuchupu ivunjike dakika ya 32, baada ya Madaraka kufunga bao ambalo kabla ya kufumua shuti lililomshinda kipa Manyika Peter, aliushika mpira kwa makusudi, ili kuuweka sawa. Rais wa Yanga wakati huo, Tarimba Abbas aliinuka na kuwaonyesha ishara wachezaji wake watoke uwanjani na hapo ndipo meza kuu aliyokuwa ameketi mzee Mwinyi, ilipoanza kushambuliwa kwa chupa za maji na mashabiki wa Yanga. Mwamuzi wa mchezo huo, Abdulkadir Omar alisubiri hadi vurugu zilipotulizwa na FFU ndipo akaendeleza mchezo. Tarimba alitoka nje na hakutaka kuendelea kushuhudia mchezo huo. Baada ya hapo, alifungiwa na Chama cha Soka Tanzania, FAT).

JULAI 2, 2005

CCM Kirumba, Mwanza. Fainali

Simba Vs Yanga, 2-0

WAFUNGAJI: Emmanuel Gabriel dk. 60, Mussa Hassan Mgosi dk. 72

AGOSTI 15, 2006

Simba Vs Yanga; Nusu Fainali, 1-1

WAFUNGAJI:

SIMBA: Emanuel Gabriel dk. 69

YANGA: Credo Mwaipopo 90

(Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 7-6)

DESEMBA 24, 2009

Yanga Vs Simba; Nusu Fainali, 2-1

WAFUNGAJI:

YANGA: Jerry Tegete dk 67, Shamte Ally dk 120

SIMBA: Hillary Echesa dk 78 (penalti)

(Uwanja wa mpya wa Taifa)

KOMBE LA MAPINDUZI:

Januari 10, 2017; Nusu Fainali

Simba 0-0 Yanga

Simba ilishinda kwa penalti 4-2

JANUARI 12, 2011

Simba Vs Yanga; Fainali 2-0

WAFUNGAJI: Mussa Mgosi dk 33, Shijja Mkinna dk 71

(Uwanja wa Amaan, Zanzibar)

KOMBE LA AICC:

JUNI 1989

Yanga Vs Simba SC 1-0

MFUNGAJI: Joseph Machella

APRILI 20, 2003,

CCM Kirumba, Mwanza

Yanga Vs Simba 3-0

WAFUNGAJI:

Kudra Omary dk. 30, Heri Morris dk 32 na Salum Athumani dk. 47

KOMBE LA CCM

JANUARI 19, 2003

Simba Vs Yanga 1-1, Dsm

WAFUNGAJI:

SIMBA: Jumanne Tondolo dk. 10

YANGA: Mwinyi Rajabu dk. 20

NGAO YA JAMII:

FEBRUARI 17, 2001

Yangs Vs Simba 2-1, Dsm

WAFUNGAJI:

YANGA: Edibilly Lunyamila dk. 47, AllyYussuf 'Tigana' dk 80.

SIMBA: Steven Mapunda 'Garrincha' dk.43

AGOSTI 18, 2010

Yanga vs Simba 0-0

(Yanga ilishinda kwa penalti 3-1)

WAFUNGAJI: Geoffrey Bonny, Stefano Mwasyika na Isaac Boakye kwa upande wa Yanga na Mohamed Banka kwa Simba.

WALIOKOSA: Ernest Boakye kwa Yanga na Emanuel Okwi, Uhuru Suleiman na Juma Nyosso kwa Simba.

AGOSTI 17, 2011

Simba vs Yanga 2-0, Dar

WAFUNGAJI:

Haruna Moshi Boban dk 15 na Felix Sunzu dk 38.

KOMBE LA FAT

NOVEMBA 15, 2000

Yanga Vs Simba 2-1

Sheikh Amri Abeid, Arusha.

WAFUNGAJI:

YANGA: Aziz Hunter 40 na Vincent Tendwa

SIMBA: Ally Yussuf 'Tigana' dk.37

NOVEMBA 12,  2000

MARUDIANO KOMBE LA FAT

Simba Vs Yanga 1-0, Dsm

MFUNGAJI:

SIMBA: Ben Luoga  dk.44       

(Matokeo ya jumla yakawa 2-2 na Yanga ikatolewa kwa mikwaju ya penalti 5-4)


No comments:

Post a Comment