Saturday 24 February 2018

BMT Yavunja Mkutano Mkuu, Yaunda Kamati BFT

Katibu Mkuu Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Mohamed Kiganja.

Na Mwandishi Wetu
BARAZA la Michezo la Taifa (BMT) limefuta Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Ndondi Tanzania (BFT) uliopangwa kufanyika leo mjini Dodoma na badala yake imeindwa Kamati ya Muda itakayoongoza mchezo huo.
Katibu Mkuu wa BMT, Mohamed Kiganja akizungumza kwa njia ya simu leo kutoka Dodoma alisema kuwa, wameshindwa kuendesha uchaguzi huo sababu Katiba ya BFT haielezi lengo la shirikisho hilo.
Mwenyekiti wa Kamati mpya ya BFT, Mutta Lwakatare.
Kiganja aliwataja wanaunda kamati hiyo ya watu sita kuwa ni pamoja na aliyekuwa rais wa BFT, Mutta Lwakatale (mwenyekiti), wakati wajumbe ni Yono Kivela, Samuel Sumwa, Lucas Muta, Aisha Viniatis na Aboubakar Mohamed.
 Aliyataja majukumu yao wanayotakiwa kuyatekeleza ndani ya miezi mitatu kuwa ni pamoja na kurekebisha Katiba, kuitisha Mkutano Mkuu wa kupitisha Katiba pamoja na kuandaa Uchaguzi Mkuu.
Mjumbe wa Kamati ya BFT, Mohamed Aboubakary.
 
Kiganja alisema kuwa pia kamati  hiyo mbali na majukumu hayo, imepewa kazi ya kuendesha na kusimamia shughuli za kila siku za mchezo huo hapa nchini.
 Akielezea sababu za kumrejesha Rwakatale wakati alikuwemo katika uongozi uliopita ambao ulishindwa kutekeleza majukumu yao, Kiganja alisema Rais wa BFT sio mtendaji,ambapo Katibu Mkuu Makore Mashaga ndiye alikuwa mtendaji na ndio maana hakurudishwa.
Mjumbe wa Kamati ya BFT, Aisha Voniatis
 Alisema kuwa kamati hiyo sasa inatakiwa kukamilisha yote hayo ndani ya miezi mitatu na kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika kipindi hicho ili kuwapata viongozi halali.


2 comments: