Tuesday 27 February 2018

Wafanyakazi JNIA, TAA Wamlilia Swai


Marehemu Jerome Swai  wakati wa uhai wake

 Na Mwandishi Wetu

WAFANYAKAZI wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) na wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) wamesikitishwa na kifo cha Bw. Jerome Swai (58) aliyekuwa fundi bomba mahiri kilichotokea  tarehe 26 , 2018 kwenye hospitali ya Amana baada ya kuugua kwa muda mfupi.

  1. Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Johannes Munanka (kulia), akimpa pole Bi. Honoratha Emmilian aliyefiwa na mume wake marehemu Jerome Swai aliyekuwa Fundi Bomba (JNIA), alifariki tarehe 26 Februari, 2018 kwenye hospitali ya Amana Jijini Dar es Salaam.

Wafanyakazi hao kwa nyakati tofauti walisema marehemu Swai alikuwa hakubali kushindwa kwa kuhakikisha anatatua tatizo linalohusiana na mabomba ya maji kwa wakati wote anapokuwa kazini.

Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Iringa, Bi. Hanna Kibopile alisema marehemu ameacha pengo kubwa kutokana na uchapakazi wake uliotukuka.

Meneja Uendeshaji wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Vedastus Fabian, akitoa pole kwa Bi. Honoratha Emmilian ambaye ni mke wa marehemu Jerome Swai aliyekuwa fundi bomba.  

Naye meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Mtwara, Bw. Daimon Mwakyosa alisema marehemu alikuwa akifanyakazi kwa bidii na hakukubali kushindwa.

“Marehemu alikuwa akiijua vyema kazi yake na hakukubali kushindwa nakumbuka wakati nikiwa JNIA na tukiwa tumepangwa shift (zamu) moja hakuna kilichoshindikana kwake kuhusu fani yake aliijua vyema kazi yake,” alisema Bw. Mwakosya.

Waombolezaji kwenye msiba wa marehemu Jerome Swai (kushoto), wakipokea pole kutoka kwa Meneja Uendeshaji wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Vedastus Fabian. Marehemu Swai alikuwa Fundi Bomba JNIA na alifariki tarehe 26 Februari 2018.

Bi. Fatma Matimba, Kaimu Meneja Utawala JNIA, alisema marehemu Swai alikuwa mchapakazi, ambapo mwaka jana alichaguliwa kuwa mfanyakazi hodari. Pia aliwahi kupewa cheti cha ufanyakazi hodari mwaka 2001 kinachotolewa TUGHE.

Ndugu wa marehemu Jerome Swai wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Johannes Munanka (mwenye tai) alipofika kuwafariji, ambapo marehemu alikuwa Fundi Bomba JNIA. 

Marehemu Swai alizaliwa mwaka 1960 wilaya ya Rombo, na kupata elimu katika shule ya msingi Kilesi mwaka 1976, na baadaye kujiunga na Chuo cha Ufundi cha Makalema akisomea fani ya ufundi bomba daraja la tatu, na baadaye kujiendeleza katika Chuo cha Ufundi cha Chang’ombe mwaka 1988 na VETA mwaka 2007.

  1. Baadhi ya Wafanyakazi wa Kiwanja cha Ndege cha Julius Nyerere (JNIA), wakiwa kwenye msiba wa marehemu Jerome Swai aliyekuwa Fundi Bomba. Swai alifariki rarehe 26 Februari 2018 katika hospitali ya Amana.

Marehemu aliajiriwa na TAA  mwaka 1984 akiwa kama fundi bomba daraja la tatu na baadaye alijiendeleza na kufanikiwa kusoma hadi kufikia daraja la kwanza. Marehemu ameacha mjane Bi. Honoratha Emmilian ambaye naye ni mfanyakazi wa TAA katika Idara ya Utawala akiwa kama mhudumu.

  1. Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Juluius Nyerere (JNIA), Bw. Johannes Munanka aliyeinama (kushoto) akiteta jambo na baadhi ya wafanyakazi wa JNIA waliofika kwenye msiba wa aliyekuwa fundi Bomba, Bw. Jerome Swai.

Mungu aipumzishe Roho ya Marehemu mahala pema peponi. Amina!

No comments:

Post a Comment