Monday 26 February 2018

Bingwa Euro 2020 kuondoka na pauni Mil34


ZURICH, Uswisi

TIMU 24 zitakazofuzu kwa mashindano ya Euro 2020 zitagawana kiasi cha Euro milioni 371, kiasi ambacho ni rekodi ya ongezeko kulinganisha na zawadi iliyopita.

Hatua hiyo imefikiwa na Shirikisho la Soka la Ulaya (Uefa) wakati wa mkutano wake mkuu uliofanyika juzi Bratislava, Slovakia.

Ongezeko ni zawadi za jumla ni asilimi 23 zaidi ya lile la zawadi za mashindano hayo yalipofanyika Ufaransa, Euro 2016, ambako kwa mara ya kwanza nchi 24 zilishiriki katika mashindano hayo.

Kila nchi itakayoshiriki itapokea kiasi cha Euro milioni 9.25 (sawa na zaidi ya Sh milioni 230) kwa ajili ya ushiriki tu, nyongeza na Euro milioni 1.5 katika kila mchezo atakaoshinda hatua ya makundi na Euro 750 000 endapo atatoka sare.

Kutakuwa bna fedha zingine zaidi katika kila raundi atayocheza hatua ya mtoano, ikiwa na maana kuwa mshindi ataondoka na kitita cha Euro milioni 20.25 mbali na zile za hatua ya makundi.

Mshindi wa Kombe la Mataifa ya Ulaya mwaka 2020 ataondoka na kiwango cha juu cha Euro milioni 34, ukilinganisha na Euro milioni 27 alizopata mshindi wa mwaka 2016.

Fainali za Euro 2020 zitapigwa katika miji 12 tofauti ya Ulaya, huku Uwanja wa Wembley jijini London ndio utakaoandaa fainali hizo zitakazofanyika Julai 12.


No comments:

Post a Comment