Tuesday 13 February 2018

Mkapa Aongoza Harambee Kuchangia Mfuko wa Ukimwi

Rais Mstaafu wa Tanzania, William Mkapa akimpongeza Meneja Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Lulu Mengele baada ya kununua picha yenye sura za marais wote wa awamu tano wa Tanzania wakati wa hafla ya kuchangia Mfuko wa Udhamini wa Kupambana na Ukimwi iliyofanyika jana usiku katika hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.Wa pili kulia ni mratibu wa shughuli hiyo, Teddy Mapunda.

Na Mwandishi Wetu
JUMLA ya Sh milioni 293 zilikusanywa na Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (Tacaids) kwa ajili ya Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi (AIDS Trust Fund) katika hafla ya kuchangia iliyofanyika katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.

Mgeni rasmi katika harambee hiyo alikuwa Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa, ambaye pia alitunukiwa ulezi wa mfuko huo, ambapo aliubali.
Mwakilishi wa GGM, Tenga Tenga (kushoto), ambaye pia ni Ofisa Uhusiano wa kampuni hiyo akipongezwa na Mkurugnzi Mkuu wa Tacaids, Leonard Maboko baada ya GGM kukbidhi mfano wa hundi yenye thamani ya Sh milioni 100 kwa Rais Mstaafu Mkapa jana usiku.
Akizungumza wakati wa ufungaji wa hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Tacaids, Dk Leonard Maboko aliwashukuru wote waliochangia, ambapo alisisitiza kuwa hakuna senti hata moja itakayotumika vibaya.

Maboko alisema kuwa fedha hizo zitasaidia kusaidia shughuli mbalimbali za mfuko huo katika mapambano yake ya ukimwi.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Tacaids, Nadhifa Omar (kushoto) na mratibu wa Harambee ya kuchangisha fedha za Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi (Aids Trust Fund), Teddy Mapunda.
Mkapa ambaye ndiye muanzilishi wa mfuko huo wakati akiwa Rais na kutangaza Ukimwi kama Janga la Taifa, jana usiku alisema kuwa mfuko huo umesaidia sana kutoa elimu kwa wananchi kuhusu tatizo la ukimwi na jinsi ya kupambana nalo.

Wakati huohuo, Kampuni ya uchimbaji madini ya Geita Gold Mine imechangia mfuko huo kiasi cha Sh milioni 100.
Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa akimkabidhi cheti mwakilishi wa GGM, Tenga Tenga katika hafla hiyo.
Mwakilishi wa GGM katika hafla hiyo, Tenga Tenga alikabidhi hundi ya thamani hiyo kwa Rais Mkapa.












 

No comments:

Post a Comment