Tuesday 13 February 2018

Sharapova Atolewa Raundi ya Kwanza Qatar Open


DOHA, Qatar
MARIA Sharapova amejikuta akitolewa katika raundi ya kwanza ya mashindano ya Qatar Open baada ya kufungwa na Mromania Monica Niculescu hapa.

Mrusi Sharapova, mwenye umri wa mika 30, alitolewa katika mashindano hayo baada ya kufungwa 4-6 6-4 6-3 katika mchezo uliodumu kwa saa mbili na dakika 38 na mchezaji anayeshikilia nafasi ya 92 kwa ubora duniani.

Sharapova, ambaye ni bingwa namba moja wazamani, alipambana kutaka kufanya vizuri, lakini alijikuta akifanya kizembe makosa 52 katika mchezo wote.

Kwa ushindi huo, Niculescu sasa katika raundi ijayo, atachesa ama na Magdalena Rybarikova au Fatma Al Nabhani ambaye hayumo katika orodha ya ubora duniani.

Sharapova, yuko katika nafasi ya 41 ya viwango vya ubora duniani, alikuwa akicheza kwa mara ya kwanza baada ya kutofuzu mashindano hayo ya Qatar tangu mwaka 2013.

Baada ya kupata seti ya kwanza katika nafasi ya nne, Sharapova alijikuta akizidiwa ujanja na Niculescu, na kupoteza mwelekeo wakati Mromania huyo akiendelea kufanya vizuri katika mchezo huo.

Muingereza Johanna Konta jana alitarajia kucheza raundi ya kwanza dhidi ya Mmarekani Bernarda Pera, ambaye alimshinda katika mashindano ya Australian Open Januari.

No comments:

Post a Comment