Tuesday 27 February 2018

Conte mbioni kuifundisha timu ya taifa ya Italia



Antonio Conte

LONDON, England


KOCHA wa Chelsea Antonio Conte ndiye chaguo namba moja la kuwa kocha wa timu ya taifa ya Italia, makamu wa rais wa Shirikisho la soka la Italia, Alessandro Costacurta alibainisha jana.

"Bado hatujachagua lakini nafikiri Conte ni mmoja wa makocha ambao wanaweza kufanya vizuri. “Miezi kadhaa iliyopita niliwahi kuzungumza naye.”

Nyota huyo wazamani wa AC Milan Costacurta ndiye aliyepewa jukumu la kumtafuta mbadala wa Gian Piero Ventura, ambaye alitimuliwa baada ya timu ya taifa ya Italia kushindwa kufuzu kwa Kombe la Dunia.

Conte, 48, aliifundisha Italia kutoka mwaka 2014 hadi kucheza robo fainali ya mashindano ya Ulaya, Euro 2016 kabla hajachukuliwa na Chelsea.

Roberto Mancini

Wengine wanaofikiriwa kuwa na uwezo wa kuifundisha Italia ni pamoja na Roberto Mancini, Claudio Ranieri na Carlo Ancelotti.

"(Conte) tayari anajua jinsi ya kuifundisha timu ya taifa ya Italia wakati wengine bado hawajahi kuifundisha, “alisema Costacurta.

Claudio Ranieri 

Conte aliiongoza Chelsea kutwaa taji la Ligi Kuu ya England katika msimu wake wa kwanza wa kuifundisha, lakini kwa sasa inashikilia nafasi ya tano katika msimamo wa ligi hiyo, pointi 19 nyuma ya vinara Manchester City.

Carlo Ancelotti

Costacurta aliendelea kusema: "Hiyo naina maana kuwa sitakuwa na furaha na Mancini au na Ancelotti – ingawa (Ancelotti) anaonekana mwenyewe amejiondoa katika mbio za kuwania kuifundisha timu hiyo.


No comments:

Post a Comment